Watu saba wamekufa huko Ethiopia
kaskazini baada ya vikosi vya usalama kufyatua risasi kwenye mkusanyiko
wa watu waliohudhuria tamasha la kidini siku ya jumamosi.
Vifo
hivyo katika mji wa Waldiya vimesababisha maandamano ya siku mbili
yaliyosababisha uharibu wa nyumba, magari na barabara kufungwa .
Mashuhuda
wanasema shida ilianza siku ya jumamosi pale waumini hao walipoanza
kuimba nyimbo za kuipinga serikali na ndipo vikosi vya serikali vilianza
kuwafyatulia risasi na kusababisha majeraha na vifo.
0 comments:
Post a Comment