Na Anitha Jonas – WHUSM
Dar es Salaam
Serikali
imetoa msisitizo kwa Klabu ya Mchezo ya Simba kuzingatia sheria na
kanuni zinayosimamia suala la uwekezaji kwa Klabu zilizoanzishwa na
wanachama ambapo wanachama wanachukua 51% na mwekezaji anachukua 49%.
Msisitizo
huo umetolewa jana jijini Dar es Salaam na Waziri wa Habari Utamaduni
Sanaa na Michezo Dkt.Harrison Mwakyembe alipokutana na uongozi wa Klabu
ya Simba na kuzungumza nao kufuatia kutoa asilimia 50% kwa mwekezaji wa
klabu hiyo Bw.Mohamed Dewji waliyemtanganza hivi karibuni ambapo ni
kinyume na sheria.
“Kanuni
zinazosimamia masuala ya udhamini kwa vilabu zilifanyiwa marekebisho
Novemba 2017 kwa ambapo ilioneka ni vyema klabu za michezo
zilizoanzishwa na wanachama wanapopata muwekezaji basi mwekezaji achukue
49% na wanachama kutoka na mchango wao kwa mkubwa kwa klabu hiyo basi
wapewe 51% lengo ikiwa ni mwanachama aweze kunufaika
vizuri,”Dkt.Mwakyembe.
Akiendelea
kuzungumza katika mkutano huo na waandishi wa habari Mheshimiwa
Mwakyembe alisema kuwa serikali ya awamu ya tano hajaja kuuwa michezo
bali lengo lake ni kuboresha michezo na kuifanya kuwa na tija zaidi
pamoja na kuleta maendeleo endelevu katika sekta hiyo.
Naye
Katibu wa Baraza la Michezo Taifa Bw.Mohamed Kiganga alieleza kuwa
ofisi yake ipo katika maandalizi ya kuwaandikia barua Klabu ya Simba ya
wapamsisitizo wa Serikali katika kuzingatia sheria katika suala la
udhamini na barua hiyo itawafikia wiki ijayo.
Kwa
Upande wa Kaimu Rais wa Klabu ya Simba Bw.Salim Abdallah alieleza
vyombo vya habari kuwa wanashukuru serikali kwa kuwaeleza kuwa milango
iko wazi pale watakapo kuwa na tatizo au watakapo hitaji ushauri
wanaweza kuonana na watendaji wake.
0 comments:
Post a Comment