Home » » KUMEKUCHA WANAWAKE MBEYA

KUMEKUCHA WANAWAKE MBEYA

Unknown | Wednesday, January 17, 2018 | 0 comments



Mamia ya wanawake wanatarajia kukutana Jijini Mbeya kwaajili ya kuadhimisha siku ya wanawake Duniani Tarehe 8/03/2018 ndani ya ukumbi wa Tugimbe saa nane kamili mchana (8:00 AM) ambapo pamoja na kukutana pia watatoa misaada kwa watoto wanaoishi katika mazingira magumu, pamoja na yatima jijini hapo.
Akizungumza na AFRICAN NEWS BLOG,Bi,LIDIA MTELIKI ambaye ndiye  mratibu wa Kusanyiko hilo,amesema kila mwaka wanawake wa jiji la Mbeya hukutana kwa lengo la kuadhimisha siku ya mwanamke Duniani katika kusanyiko hilo huwa na mambo kadhawakadha ikiwemo kuendesha semina ya ndoa,kutoa misaada kwa wasio jiweza,watoto waishio katika mazingira magumu pamoja na yatima.
Bi,Mteliki ameongeza kuwa  siku hiyo kutakuwa na Walimu walio bobea katika kutoa Elimu ya maisha ya mwanamke katika ndoa pamoja na burudani, pia wanawake watapewa fulsa ya kutoa mawazo yao katika kuelekea nchi ya viwanda na uchumi wa kati katika kumwinua mwanamke.
Aidha Bi,Lidia Mteliki ametowa wito kwa wanawake wote kushiriki kusanyiko hilo,huku akibainisha mikoa na nchi zitakazo shiriki ikiwemo,mikoa ya Mbeya, Arusha,Iringa,Songea,Rukwa pamoja na nchi za Malawi,Zambia nk.

Share this article :

0 comments:

Post a Comment

 
Support : Copyright © 2018. AFRICAN NEWS BLOG - All Rights Reserved
Imetengenezwa na Edwin Moshi
Inaendeshwa na AFRICAN NEWS BLOG