Askofu
Mkuu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima leo Januari 21,
2018 amepata pigo kwa kuondokewa na mama yake mzazi Bi. Ruth Basondole
Gwajima ambaye amefariki asubuhi ya leo.
Gwajima
amesema kuwa mama yake mzazi amefariki akiwa na umri wa miaka 84 na
kuwa mazishi ya mama yake mpendwa yatafanyika siku ya Alhamisi ya
Januari 25, 2018 siku ya Alhamisi Salasala jijini Dar es Salaama.
"Leo
Saa mbili asubuhi mama yangu Mzazi, Bi Ruth Basondole Gwajima
ametwaliwa na Bwana. Karudi Mbinguni akiwa na Umri wa Miaka 84. Kuna
Furaha ya Ajabu Shujaa Wangu Amerudi kwao. Kwasababu katika maisha yake
alimtumikia Mungu. Mazishi yatafanyika Alhamis Tarehe 25/01/2018;
Salasala Dar es Salaam" alisema Gwajima
0 comments:
Post a Comment