Home » » Tucta wamuomba Rais kuongeza mshahara kima cha chini

Tucta wamuomba Rais kuongeza mshahara kima cha chini

Unknown | Tuesday, May 01, 2018 | 0 comments
Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA) limemuomba Rais John Magufuli kuangalia namna ya kuongeza mshahara wa kima cha chini angalau kisiwe chini ya Sh250, 000.

Hayo yamesemwa leo Mei Mosi na Katibu Mkuu wa Tucta, Dk Yahaya Msigwa wakati wa sherehe za wafanyakazi, zinazoadhimishwa kitaifa katika viwanja vya Samora mkoani Iringa, ambapo Mgeni Rasmi ni Rais John Magufuli.

Amesema maisha kwa walio wengi yanakuwa magumu kutokana na kupanda kwa bei za vitu muhimu ikiwemo vyakula na huduma za msingi za maisha.

“Tunaomba Rais wetu kima cha chini kisipungue 250,000 kwa mwezi , lakini pia tunaiomba Serikali kubuni vyanzo vingine vya mapato ili kuongeza wigo wa utoaji huduma kwa watumishi au wafanyakazi, kuna mfanyakazi anapata Sh100,000 hii haitoshi kitu kwa mtu mwenye familia yenye watoto wanne,” amesema Dk Msigwa.

Aidha alitoa wito kwa Serikali kuangalia upya namna ya kubuni vyanzo vingine vya mapato ili kupunguza machungu kwa wafanyakazi kwani wanakatwa kodi kubwa.

Share this article :

0 comments:

Post a Comment

 
Support : Copyright © 2018. AFRICAN NEWS BLOG - All Rights Reserved
Imetengenezwa na Edwin Moshi
Inaendeshwa na AFRICAN NEWS BLOG