Home » » Mzee Majuto azidiwa, arudishwa hospitali

Mzee Majuto azidiwa, arudishwa hospitali

Unknown | Monday, April 23, 2018 | 0 comments
Muigizaji na mchekeshaji wa siku nyingi, Amri Athuman maarufu Mzee Majuto, amelazwa tena katika Hospitali ya Tumaini jijini Dar es Salaam, baada ya kuzidiwa.

Mke wa mwigizaji huyo, Aisha  Yusufu, ameiambia MCL Digital leo Aprili 23  kwamba mume wake walimpeleka hospitalini hapo leo saa 7:00 mchana.

Aisha amesema kidonda alichofanyiwa upasuaji kimeleta shida, hivyo kumpeleka kwa ajili ya uangalizi zaidi.

Majuto alilazwa hospitalini hapo Januari mwaka huu na kufanyiwa upasuaji wa tezi dume.

Share this article :

0 comments:

Post a Comment

 
Support : Copyright © 2018. AFRICAN NEWS BLOG - All Rights Reserved
Imetengenezwa na Edwin Moshi
Inaendeshwa na AFRICAN NEWS BLOG