Home » » Msanii Godlucky Haamini kukutana na Raisi na Kumpa Mkono.

Msanii Godlucky Haamini kukutana na Raisi na Kumpa Mkono.

Unknown | Friday, April 13, 2018 | 0 comments
Mwanamuziki anaefanya vizuri katika nyimbo za injili, Godlucky Gosbeth amefunguka na kusema kuwa hakuamini alipokuatana na raisi katika sherehe za uzinduzi wa taasisi ya Jakaya  Kikwete  iliyofanyika juzi   jijini Dar es salaam.

Godlucky anasea kuwa kwake ni bahati sana  na hakutegemea kama angeitwa pale mbele kwa ajili ya kusalimiana na viongozi wakubwa wa serikalai mpaka alipotoka ikulu ndipo alipoaanza kuamini kuwa ni kweli jambo lile limetendeka.

Godluck  anasema kuwa , kuonekana kwake na kusalimiana  na viongozi wakubwa imemfanya apokee simu nyingi sana zikimpongeza kwa kazi hiyo nzuri aliyoifanya na hata yeye pia anashukuru Mungu kwa kuwa anazidi kumbariki.Godlucky aliyaongea hayo alipokuwa akiongea na radio clouds fm.

Hata katika ukurasa wake wa instagram , Gudluck aliandika maneno ya kumshukuru Mungu kwa kuandika kuwa katika maisha yake hakuwahi kuwaza kama kuna mambo makubwa kama hayo yangeweza kutokea katika maisha yake lakini anachoamini ni kwamba Mungu amekuwa akitimiza ahadi alizokuwa ameweka kumtimizia maishani mwake.
Share this article :

0 comments:

Post a Comment

 
Support : Copyright © 2018. AFRICAN NEWS BLOG - All Rights Reserved
Imetengenezwa na Edwin Moshi
Inaendeshwa na AFRICAN NEWS BLOG