Home » » Makalio Yampatia Aunty Lulu Wachumba Watatu

Makalio Yampatia Aunty Lulu Wachumba Watatu

Unknown | Friday, April 13, 2018 | 0 comments
Mtangazaji na muigizaji wa Bongo movie Lulu Semagongo maarufu kama aunty Lulu amewaacha watu wengi midomo wazi baada ya kudai kalio lake kubwa limemsaidia kupata wachumba watatu nchini China.

Kwenye mahojiano na Global Publishers Aunty Lulu alifunguka na kudai kuwa kwenye Safari yake ya kibiashara nchini China hivi karibuni alihudhuria kwenye ukumbi mmoja ambao kulikuwa na msanii ambaye ni Mtanzania ambaye alikuwa anapiga shoo.

Aunty Lulu amedai baada ya muziki kuanza kupigwa alianza kucheza na kukata mauno kiasi ya kwamba wanaume walianza kumtolea macho na usiku huo alipata wachumba watatu ambao wapo tayari kumuoa.

"Kalio langu limenipatia wachumba wa Kichina watatu, sasa baada ya wote kuniambia wanataka kunioa, niliwatajia mahari yangu kuwa ni shilingi milioni 50 na walikubali, lakini niliwapa mtihani mwingine kwamba atakayekuwa wa kwanza kufika Bongo ndiye atakayenioa, hivyo ninasubiri na ndoa yangu itakuwa ya mkataba”.
Share this article :

0 comments:

Post a Comment

 
Support : Copyright © 2018. AFRICAN NEWS BLOG - All Rights Reserved
Imetengenezwa na Edwin Moshi
Inaendeshwa na AFRICAN NEWS BLOG