Home » » Kuhusu Kuchanjwa Chale Na Wachawi

Kuhusu Kuchanjwa Chale Na Wachawi

Unknown | Tuesday, April 24, 2018 | 2comments
NA. DOKTA  MUNGWA  KABILI. ….0744  000  473.
Katika  maeneo  mengi  ya  vijijini  ni  jambo  la  kawaida  sana kwa watu  kuamka na kujikuta  wakiwa  wamechanjwa  chale  sehemu  mbalimbali  mwilini na  wasijue  chale  hizo  wamechanjwa  na  nani na  kwa  sababu  gani.

Jambo hili  halitokei maeneo ya  vijijini  tu  bali hutokea  na mijini  pia.

Watu  huamka  asubuhi  na  kujipata  wakiwa  wamechanjwa  chale  bila  kujua  ni  nani  aliehusika  na  kuwachanja  chale  hizo  na  alifanya  hivyo  kwa  sababu  gani.

Katika  makala  ya  leo  tutapata  kuwafahamu  ni  akina  nani  haswa  wanao  wachanja  watu  chale  usiku  wakiwa  wamelala  na  huwa  wanafanya  hivyo  kwa  sababu  gani.

Kwanini  wachawi  huwachanja  watu  chale  usiku ?

Wachawi  huwachanja  watu  chale  kwa  sababu  mbalimbali. Baadhi  ya  sababu  hizo  ni  kama  ifuatavyo :

1.   KUSOMA  NYOTA  ZA  WAHUSIKA : Story  ya  maisha  ya kila  mtu huwa  imeandikwa  kwenye  damu  yake .

Kwa  kutumia  maarifa  ya  juu  kabisa  ya  kichawi, wachawi  wanaweza kusoma  story nzima ya  maisha  ya  mtu  kwa  kutumia  damu  yake.

Kwa lugha  nyepesi ni kwamba  katika  ulimwengu  wa  rohoni  damu  ya  mtu  ni kama  ubao  ama  kitabu  ambacho  kimeandiwa story nzima  ya maisha  ya  mtu  huyo.

Siri  na  mipango  yote  ya maisha  ya  mwanadamu  ambayo  amepangiwa  na  Mwenyezi  Mungu  imeandikwa  katika  damu  yake.

Wachawi  wakitaka  kujua  kuhusu  siri  hii  huhaha  kutafuta  damu ya mtu  ambae  wanataka  kujua  kuhusu  maisha  yake.

Hivyo  basi  wachawi  wanavyo mchanja mtu  chale, pamoja  na  mambo mengine, hufanya  hivyo  kwa lengo la  kupata damu  ambayo  wataitumia kusoma  nyota  ya  mhusika.

KAMA  AMBAVYO  WATAALAMU WA  KISAYANSI  WANAWEZA  KUJUA  MAISHA  YA  MTU  YAKOJE  KWA  KUMFANYIA  MTU  HUYO  KIPIMO  KIITWACHO  FULL BLOOD  PICTURE, BASI  VIVYO  HIVYO  WACHAWI  WANAWEZA  KUJUA  SIRI  YA  MAISHA  YA  MTU  KWA KUTUMIA  DAMU  YAKE.

NAOMBA  NIELEWEKE  VIZURI  KUHUSU  KIPIMO  CHA  FULL BLOOD  PICTURE  NA  KUJUA  MAISHA  YA  MTU.

 SIMAANISHI  KWAMBA  KWA  KUMFANYIA  MTU  FULL  BLOOD PICTURE MADKATARI  WANAWEZA  KUJUA  MAISHA  YA MTU  HUYO  YATAKUWAJE  HAPO  MBELENI  LA  HASHA.

 NINA  MAANISHA  HIVI, KIPIMO  CHA  FULL  BLOOD PICTURE  NI  KIPIMO  KINACHO ONYESHA  HALI  HALISI  YA  AFYA  YA  MWANADAMU  NA  KAMA TUJUAVYO  MAISHA  NI  AFYA  NA  AFYA  NDIO  MAISHA.

KWA  KUFANYA  FULL  BLOOD  PICTURE  MADAKTARI  WANAWEZA  KUBAINI  KAMA MHUSIKA  ANA VIRUSI  VYA  UKIMWI, KISUKARI, PRESHA,SHINIKIZO   LA  DAMU, LEHEMU MWILINI  NAKADHALIKA.

WANAWEZA  KUJUA  KAMA  MTU  NI  MGONJWA  AU  ANA  AFYA  NJEMA.

NA KWA  KUJUA  KAMA  MTU  NI  MZIMA  BUKHERI  WA  AFYA  AU  ANASUMBULIWA  NA  MARADHI  MAZITO  NDANI  YA MWILI  WAKE  NI  SAWA  NA  KUJUA  KUHUSU  MAISHA  YAKE  KWA  SABABU  MAISHA  YA  MTU  NI  AFYA  NA  AFYA  NDIO  MAISHA  YA  MTU. UKIACHILIA  MIPANGO  YA MUNGU NA SHARI  ZA WACHAWI, AFYA  YA MTU NDIO INAYO AMUA UMRI WA MTU KUISHI.  UHAI  WA  MTU  UPO  KWENYE  DAMU  YAKE.

Vivyo  hivyo  basi  wachawi  wanapo taka  kujua  siri  za  maisha  ya  mtu  hufanya  hivyo  kwa kutumia  damu  yake. Hii ni  kwa  sababu  maisha  ya  kila  mwanadamu  yameandikwa  kwenye  damu  yake. Siri  zote  kuhusu  maisha  ya  kila  mtu  zimefichwa  kwenye  damu  yake.

2.   KUIBA  NYOTA  : Hii  ni  sababu  nyingine  kwanini  wachawi  huwachanja  watu  usiku  wakiwa  wamelala. Hufanya  hivyo kwa  lengo  la  kuiba  nyota  zao.  Suala  la  kuiba  nyota  huja  baada  ya kusoma  nyota  ya  mhusika  kupitia  damu  yake na  kuona  inafaa  kuchukuliwa  kwa  matumizi  mbalimbali  kama  vile  biashara, mali nakadhalika.

3.   KUPIMA KINGA  YA  MTU : Kama  nilivyo  eleza  hapo  juu  kuwa ndani  ya  damu  ya  mtu  ndimo  kumefichwa  kila  kitu  kuhusu mtu  huyo.

Kila  siri  inayo  muhusu  mwanadamu, imeandikwa  ndani  ya  damu  yake .

Wachawi  wanapo  taka  kupima mtu  fulani  ana  kinga  kubwa  kiasi  gani hufanya  hivyo  kwa kusoma  damu  yake  au  vitu  vya  mtu  huyo  ambavyo  vimetokana  na  msukumo  wa  damu  kama  vile  manii n.k.

Kumbuka  kuwa  kinga  yoyote  ile  ya  mtu  huwa  inakaa  kwenye  damu  yake. Dawa  anazo  chanjwa  mtu  kwa  ajili  ya  kinga, dawa  anazo  kula  ama  kunywa  mtu  kwa  ajili  ya kinga  huwa  zinaenda  kukaa  kwenye  damu yake.

Sasa  basi katika  uchawi  njia  ya  juu  kabisa  ya  kujua  kinga  ya  mtu  ikoje  ni  kusoma  damu  yake.

Hivyo basi   wachawi  wanapo mchanja  mtu  chale, pamoja  na  mambo mengine, hufanya  hivyo  kwa  lengo  la  kupima  kinga  ya  mtu  huyo..

Na  lengo  la  kutaka  kujua  kinga  ya  mtu  ni kujua  mtu  huyo  kinga  yake  ina  nguvu  kiasi  gani  na  wakisha  jua  nguvu  ya  kinga  ya  mtu  huyo  kitakacho  fuatia  baada  ya  hapo  ni  kutuma  uchawi  wa  kuteketeza  kwanza  kinga kisha  ili  wapate  urahisi  au  mwanya  wa  kutupa  uchawi  wao  kwa  mtu  waliemkusudia.

4.    KUPANDA  MAPANDO  YA  KICHAWI :  Inaeleweka  vyema  kwa  wengi  kuwa  mwanadamu  aliumbwa  kwa udongo.

Wachawi wana amini  sana   katika  jambo  hili. Wao  hawaishii  tu  kuamini  kuwa  mwanadamu  aliumbwa  kwa  udongo bali  wanaenda mbele  zaidi  na  kumtreat  mwanadamu  kama udongo  kabisa.

Na  katika  kudhihirisha  hilo  kwa  vitendo, wachawi  wanaweza  kuutumia  mwili  wa  mwanadamu  kupanda  mapando  yao  mbalimbali.  Wachawi  wanaweza  kuutumia  mwili  wa  mwanadamu  ( ambao  ni  udongo) kama  shamba  la kupanda  mapando  yao.

 Mapando  yao  yanaweza  kuwa  kwa  faida  yao  wao  kama  wachawi  huku  mtu  huyo  wakimtumia  kama  shamba  tu  au  yanaweza  kuwa  kwa  ajili  ya  mtu  huyo  ili  baadae aje  ayavune katika  maisha  yake  halisi.

Ndani  ya  mwili  wa  mwanadamu  inaweza  kupandwa  roho  ya  mauti  ambayo  itakuwa  inakua  kadri  mwanadamu  anavyo  kuwa  na  anaweza  “ kula  matunda” ya  roho  hiyo  hata  baada  ya  miaka  ishirini. Inaweza  kupandwa  roho  ya  kukataliwa, roho  ya  umasikini, ufukara  nakadhalika.

Kwa  hiyo chale  hizo  zaweza kuwa  ishara  kwamba  wachawi  walikuwa  wanalima  kwenye  mwili  wako  na  kupanda  mapando  yao  ya kichawi  kupitia    damu yao.

5.   KUFUGIA  MAJINI  WACHAFU : Wachawi  wanaweza  kuutumia  mwili  wa  mtu  kama  banda  la  kufugia  majini  wachafu  ambao  watakuwa  wanawachukuwa  kuwatumia  kila  watakapo  wahitaji.,Majini  hao  wachafu  wanaweza  kukaribishwa  kwenye  mwili  wa  mtu  kupitia  chale hizo  za  kichawi.  Chale hizo  hutumika  kama  Antenna  za  kuwavuta  majini wachafu  ndani  ya  mwili  wa  mtu  walie mkusudia.

6.   KUMPAKA  MTU  NUKSI NA  MIKOSI: Kama  nilivyo  sema  hapo  awali  kuwa  story  ya  maisha  ya  kila  mtu  huwa  imeandikwa  kwenye  damu  yake.

Kuna  kanuni  moja  kubwa  sana  katika  ulimwengu  wa  rohoni  ambayo  inasema  chochote  utakacho  kiunganisha  na  damu  ya  mtu  basi  kinamezwa  na  kuwa  sehemu  ya  damu  ya  mtu  huyo  na  kitu  hicho  kikisha  kuwa  sehemu  ya  damu  ya  maisha  ya  mtu  huyo  basi  kinakuwa  sehemu  ya  maisha  ya  mtu  huyo  na  kikisha  kuwa  sehemu  ya  maisha  ya  mtu  huyo  basi  kitaanza  kujidhihirisha  chenyewe  katika  maisha  ya  mtu  huyo.

  Hii  ni  kwa  sababu  damu  ndio  nishati  inayo endesha  maisha  ya  mtu. Nishati  hii  ndio  inayo  amua  kila  kitu  katika  maisha ya  mwanadamu.

Wachawi  kwa  kulitambua  hilo, huwa  wanafanya  uchawi  maalumu  wa  kuunganisha  damu  ya  mtu  na  vitu  vibaya ili  vitu  hivyo  vibaya  na  vichafu  vikafanyike  kuwa  sehemu  ya  damu  ya  mtu  huyo  na  hivyo  kuharibu  utaratibu  mzima  wa  maisha  ya  mtu  huyo.

Hufanya  hivyo  kwa  kuwatia watu  nuksi.Nuksi  hiyo  inaweza  kuingizwa  kwenye mfumo  wa  maisha  ya  mtu  kwa  njia nyingi   sana, kubwa  kuliko  zote  ni  njia  hiyo  ya  kuwachanja  chale  na  kuwapaka nuksi.

Nuksi  sio  neo  tu  kama  baadhi  ya  watu  wanavyo  lichukuliwa. Sio  neno  wala  msemo.

Ni uchawi  kabisa  ambao  nguvu  yake  hubeba  maudhui  ya  jina  lake. Zipo  nuksi za  aina  nyingi  sana.

 Moja  wapo  kati  ya  nuksi  hizo  ni  nuksi  inayo  tengenezwa  kwa  vitu  mbalimbali  kama  vile : Mavi  ya  mtu  fresh ambayo  alijisaidia  akiwa  porini, mavi  ya  nyani, mavi ya sokwe, mavi ya  chatu, mavi ya kenge, uchafu  wa  kwenye  majalala  saba ( Wakati  uchafu  huu  unachukuliwa  hufanyika  tambiko  maalumu  la  kichawi  linalo  husisha  kafara  ya  mnyama  au  ndege, ambayo  hulenga  katika  kuwaamsha  majini  wachafu  walio  lala  katika majalala  hayo  kuingia  ndani  ya  uchafu  huo), kipande  cha  mti kilicho  okotwa  ndani ya  kaburi wakati  kaburi  linachimbwa, utumbo  wa  kuku, maji yaliyo tumika kuoshea  maiti, uchafu  wa  mochwari, shahidi  la  kaburi, dawa  moja  ya  kiarabu  ifananayo  na  lami  na yenye  kutoa  harufu  mbaya  sana , uchafu  wa chooni pamoja na  madawa  mengine  ya  kichawi  ambayo  ninayahifadhi  hapa)

Vitu  vyote  hivyo vinapikwa  kwa  pamoja  kwa  kutumia  dawa  ya  paka  mweusi.

Vinakaangwa  hadi  kuwa  majivu  halafu  mhusika  anaenda  kupakwa  kichawi  usiku.

Wakati  mwingine  zoezi  la  kumpaka  mtu  nuksi  huweza  kuendana  na  zoezi  la  kumpaka  damu  mbichi  ya  mnyama  mmoja  apendwae  sana na  wachawi…

Damu  hii  hunuizwa  kutamka  mambo yatakayo  enda  kubatilisha mambo  yote  mazuri  yaliyo  andikwa  kwenye  damu  ya  mhusika.

Damu  ya  mnyama  huyu  huenda  kufuta  kila  kitu  kizuri  kilicho andikwa  kwenye  damu  ya  mtu  aliekusudiwa  na badala  yake yenyewe  ndio hukaa na  kuweka  tamko  jipya  juu  ya  maisha  ya  mtu  aliekusudiwa.

Matokeo  yake  mtu  huyo  huanza  kuandamwa  na nuksi  mabalaa  na  mikosi .
 
Makala  haya  yameandaliwa  na  Dokta. Mungwa  Kabili  ambae  anapatikana  kwa  SIMU  NAMBA  : 0744  000  473.
Share this article :

2 comments:

Post a Comment

 
Support : Copyright © 2018. AFRICAN NEWS BLOG - All Rights Reserved
Imetengenezwa na Edwin Moshi
Inaendeshwa na AFRICAN NEWS BLOG