Home » » Wafungwa waliosamehewa Tanzania wamshukuru Magufuli kwa kumwimbia

Wafungwa waliosamehewa Tanzania wamshukuru Magufuli kwa kumwimbia

Unknown | Wednesday, January 03, 2018 | 0 comments


Rais wa Tanzania John Magufuli amekutana na wanamuziki wawili aliowasamehe takriban wiki tatu zilizoita, licha ya kuwa walikuwa wanatumikia kifungo cha maisha jela kwa kuwabaka wasichana 10 wa shule mwaka 2003.
Nguza Viking, anayefahamika pia kama Babu Seya, na mtoto wake Johnson Nguza, ambaye pia anafahamika kama Papii Kocha, walimshukuru Rais Magufuli kwa kuwasamehe ambapo walimwimbia wakati walimtembelea katika Ikulu.
Gazeti la Citizen lilimnukuu Magufuli akisema, "msinishukuru mimi, bali mshukuru Mungu ambaye ndiye pekee aliye na nguvu za kusamehe".
Watetesi wa haki za watoto walikosoa msamaha huo.
Walikuwa wametumikia kifungo cha miaka 13 wakati waliachiliwa kwa kuwabaka wasichana walio kati ya umri wa miaka 6 na 8.
Wawili hao walikuwa miongoni mwa wafungwa 61 waliopata msamaha wa rais wakati wa hotuba yake ya uhuru.
Share this article :

0 comments:

Post a Comment

 
Support : Copyright © 2018. AFRICAN NEWS BLOG - All Rights Reserved
Imetengenezwa na Edwin Moshi
Inaendeshwa na AFRICAN NEWS BLOG