Home » » WANANCHI WATAADHALISHWA JUU YA KUPELEKA WATOTO SHULE

WANANCHI WATAADHALISHWA JUU YA KUPELEKA WATOTO SHULE

Unknown | Wednesday, January 03, 2018 | 0 comments



Wazazi na walezi ambao hawatawapeleka watoto shule za Sekondari kukiona cha Moto Kijiji cha Ihanga kata ya Ukwama Wilayani Makete Mkoani Njombe
M/kiti wa Kijiji cha Ihanga Fedenicko Ndelwa amesema hayo akizungumza na Kitulo Radio Fm mapema wiki hii ambapo amewataka wazazi kuwapeleka watoto shule waliochaguliwa kujiunga na Masomo ya Sekondari
Amesema hatua za kisheria zitafuatwa kwa mzazi au Mlezi ambaye hatatimiza wajibu wake wa kumpeleka motto shuleni
‘‘Nitamke wazi suala la wazazi au walezi ambao watashidwa kuwapeleka watoto wao shuleni mwezi huu January,hawa nitawasimamia kidete mpaka nahakikisha wanafunzi wanapelekwa shule’’
‘‘Halmashauri ya kijiji hiki cha Ihanga ilikaa wiki iliyopita na ikajadili kwamba kila mtoto ambaye anakuta amefaulu lazima mzazi awajibike kumpeleka Mwanaye shule kwa kuwa mzazi hilo ni jukumu lake la kisheria,hivyo sisi tutafuata sheria’’
‘‘Kijiji change kina Jumla ya Vitongoji vitano na Kila Kitongoji kwenye Mtaa wake anaidadi ya wanafunzi waliofaulu kwenda Sekondari hivyo wanahakikisha mzazi/Mlezi anapeleka Mwanaye shule’’
Kwa upande wake Afisa Elimu Sekondari Wilaya ya Makete Mwalimu Jackob Meena amesema suala la Elimu ni muhimu kwa watoto bila kubagua Jinsia,hivyo wazazi watambue jukumu la kuwasomesha watoto ni lao
Pia amesema wazazi wanatakiwa kuwa karibu sana na watoto wao wa kike kwa kuwasaidia mahitaji muhimu ili wasirubuniwe na wavulana na kuwasababishia kushindwa kuendelea na Masomo
‘‘Nilitaka nikazie kwa watoto wa kike na wakiume Elimu ndio inaweza kuwasaidia katika kujikomboa na Mazingira Magumu yanayowakabili’’
‘‘Katika Elimu tunamambo matatu makuu ambayo tunapambana nayo ikiwemo Ujinga,Maradhi na Umaskini sasa bila Elimu kupambana na hivyo vitu vitatu haiwezekani itakuwa ni kazi ngumu sana’’
‘‘Hivyo Wazazi na walezi naomba Muhakikishe watoto hawa wanapelekwa shule kwa kutambua umuhimu huo wa Elimu’’
Share this article :

0 comments:

Post a Comment

 
Support : Copyright © 2018. AFRICAN NEWS BLOG - All Rights Reserved
Imetengenezwa na Edwin Moshi
Inaendeshwa na AFRICAN NEWS BLOG