Home » » Serikali ya DRC yatangaza siku mbili za maombolezo kuwakumbuka watu waliopoteza maisha

Serikali ya DRC yatangaza siku mbili za maombolezo kuwakumbuka watu waliopoteza maisha

Unknown | Sunday, January 07, 2018 | 0 comments
Serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo imetangaza siku mbili za maombolezo kati ya Jumatatu na Jumanne wiki ijayo, kuwakumbuka watu 44 waliopoteza maisha katika mafuriko makubwa yaliyotokea wiki hii jijini Kinshasa.

Mbali na mauaji hayo, makaazi ya watu 5,000 yamejaa maji, huku makaazi mengine 192 yakiharibika ikiwa ni pamoja na kuvunjika kwa madaraja na barabara.

Maeneo yaliyoathiriwa zaidi na mafuriko hayo ni pamoja na Ngaliema, Bandalungwa, Barumbu, Limete na Selembao.
Jiji la Kinshasa limeendelea kukabiliwa na mafuriko mara kwa mara mvua inaponyesha kutokana na miundo mbinu mibaya hasa mitaro ya kupitisha  maji na msongamano wa makaazi ya watu.

Maakazi mengi ya watu yamejengwa katika maeneo ya milima, katika eneo hilo lenye watu Milioni 10.
Share this article :

0 comments:

Post a Comment

 
Support : Copyright © 2018. AFRICAN NEWS BLOG - All Rights Reserved
Imetengenezwa na Edwin Moshi
Inaendeshwa na AFRICAN NEWS BLOG