Home » » Daktari nchini Kenya akwenda Mahakamani kutaka ukeketaji kuruhusiwa

Daktari nchini Kenya akwenda Mahakamani kutaka ukeketaji kuruhusiwa

Unknown | Thursday, January 18, 2018 | 0 comments


Daktari mmoja nchini Kenya amekwenda Mahakamani mjini Machakos kutaka kuhalalishwa kwa ukeketaji wa wanawake miongoni mwa jamii zinazotekeleza utamaduni huo.
Ukeketaji ni marufuku nchini Kenya, na yeyote anayekamatwa akijihusisha hufungwa jela miaka mitatu au kutozwa faini ya Dola za Marekani 2,000.
Wanaharakati wanaopinga ukeketaji wanasema kuwa zoezi hilo, limeendelea kukiuka haki za wanawake na kuwaletea madhara ya kisaikolojia.

Hata hivyo, Daktari Tatu Kamau anasema kuwa, sheria hiyo inakiuka haki za kitamaduni za wanawake katika jamii zinazotekeleza ukeketaji kwa lengo la kudumisha mila zao.
Aidha, amesema haijawahi kuthibitishwa kuwa kuwepo kwa madhara yoyote ya kiafya kutokana na zoezi hilo na hivyo kuwabagua wanawake.

Mahakama itasikiliza ombi  hilo mwezi Februari.
Share this article :

0 comments:

Post a Comment

 
Support : Copyright © 2018. AFRICAN NEWS BLOG - All Rights Reserved
Imetengenezwa na Edwin Moshi
Inaendeshwa na AFRICAN NEWS BLOG