Home » » Uingereza yachangia euro Milioni 50,5 kwa usalama wa Calais

Uingereza yachangia euro Milioni 50,5 kwa usalama wa Calais

Unknown | Thursday, January 18, 2018 | 0 comments
Serikali ya Uingereza imetangaza leo Alhamisi, Januari 18 kwamba inaongeza euro Milioni 50,5, mchango wake wa kifedha kwa eneo la Calais na pwani za Ufaransa ili kuimarisha usalama mpakani.
Tamko rasmi kabla ya ziara ya rais wa Ufaransa Emmanuel Macron nchini Uingereza kwa mkutano wa nchi mbili kuhusu masuala ya usalama wa mipaka na ulinzi.
Ishara ya kifedha iliyotolewa na serikali ya Theresa May inakutana na matarajio yaliyoelezwa na Ufaransa ambayo inashtumu kwa miaka kadhaa suala la mikataba ya Touquet, huku shinikizo la uhamiaji limeongezeka katika Calais, ambapo uliopo mpaka wa Uingereza tangu 2004.
Euro milioni 50 iliyoahidiwa inapaswa kutumika kuboresha hatua za usalama katika bandari ya Calais na maeneo jirani. Uingereza imetumia euro milioni 113 katika kipindi cha miaka mitatu iliyopita na kutambua kuwa mikataba ya Touquet ni manufaa sana kwa nchi hiyo.
Hata hivyo, viongozi wengine wa Uingereza tayari wamekosoa mchango huo kama vile Mbunge wa chama cha kihafidhina kutoka Dover ambaye amebaini kwamba London tayari imetoa "mamilioni kwa Ufaransa" na inpaswa kuwekeza katika usalama wa mpaka kwenye pwani za Uingereza.
Hali hii itampelekea Theresa May na Emmanuel Macron kusaini mkataba mpya ambao utakamilisha mikataba ya Touquet.
Kwa ombi la Ufaransa, London pia imekubali kuhudumia wahamiaji wengi wanaokuja Calais, ikiwa ni pamoja na watoto wadogo. Viongozi hawa wawili pia watajadili kuhusu masuala ya kijeshi ili kuonyesha kwamba licha ya Uingereza kujitoa katika Umoja wa Ulaya, msikamano wa pamoja utaendelea na utaimarishwa. Uingereza pia imetangaza kutumwa kwa helikopta tatu za Royal Air Force na wafanyakazi ili kusaidia vikosi vya Ufaransa katika eneo la Sahel.
Share this article :

0 comments:

Post a Comment

 
Support : Copyright © 2018. AFRICAN NEWS BLOG - All Rights Reserved
Imetengenezwa na Edwin Moshi
Inaendeshwa na AFRICAN NEWS BLOG