Polisi
Kikosi cha Viwanja vya Ndege jijini Dar es Salaam linamshikilia raia wa
Nigeria akituhumiwa kupatikana na dawa za kulevya aina ya Cocaine.
Christian
Ugbechi (26), anadaiwa kukamatwa katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa
kwa Julius Nyerere (JNIA) akiwa na pipi 59 zenye uzito wa zaidi gramu
800.
Kamanda
wa Polisi wa Viwanja vya Ndege, Matanga Mbushi amesema leo Jumatatu
Januari 29,2018 kuwa mtuhumiwa anaishi na kufanya kazi nchini Ufaransa.
Amesema alikuwa akisafirisha dawa hizo za kulevya kwenda nchini Ufaransa.
"Tumemkamata
mtuhumiwa akiwa na pipi 59, kati ya hizo 56 alizificha kwenye soksi na
tatu amezitoa leo kwa njia ya haja kubwa. Yupo chini ya uangalizi
maalumu,” amesema Mbushi.
0 comments:
Post a Comment