Home » » Mwigulu: Watanzania Dumisheni amani

Mwigulu: Watanzania Dumisheni amani

Unknown | Monday, December 25, 2017 | 0 comments
Seebait.com 2017SeeBait
Ikiwa leo Wakristo duniani kote wanaadhimisha sikukuu ya Krismas, Waziri wa Mambo ya Ndani Mh. Mwigulu Chemba amewataka Watanzania kusherekea sikukuu za mwisho wa mwaka kwa Amani na Upendo

Waziri Mwigulu ambaye wizara yake ndio ina dhamana ya kusimamia amani na usalama wa raia na mali zao nchini ametoa salamu zake za sikukuu huku akiwakumbusha wananchi kuzingatia Amani.
Kupitia Ukurasa wake wa mtandao wa Twitter, Mh Mwigulu ameandika, “Merry Christmass & Happy New Year, tusherekee kwa Amani na Upendo”. 
Mbali na Waziri Mwigulu kusisitiza Amani kipindi hiki cha sikukuu, hivi karibuni pia Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Simon Sirro aliwataka Watanzania kusherehekea sikukuu bila kuvunja sheria za nchi.
Share this article :

0 comments:

Post a Comment

 
Support : Copyright © 2018. AFRICAN NEWS BLOG - All Rights Reserved
Imetengenezwa na Edwin Moshi
Inaendeshwa na AFRICAN NEWS BLOG