Home » » HATIMAYE SHULE YA SEKONDARI ISAPULANO YAPATA USAJILI

HATIMAYE SHULE YA SEKONDARI ISAPULANO YAPATA USAJILI

Unknown | Friday, December 29, 2017 | 0 comments




Mbunge wa jimbo la Makete Profesa Norman Adamson Sigara King ametoa machango wa bati 150 ikiwa ni kuchangia ujenzi wa madarasa na nyomba ya mwalimu ktika shule ya sekondary isapulano inayotarajiwa kuanza rasmi tarehe 8 januali 2018.
Akiongea na wananchi wa kata ya isapulano Mh.sigara amewapongeza wananchi  kwakujitolea nguvu zao kujenga shule hadi kufikia hatua ya kupata usajili ambapo amesema tayali shule hiyo ieshapangiwa wanafuzi 40.
Katika hatua nyingine mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya makete bw,fransic namaumbo masema kupata usajili wa shule kunategemea ushirikiano wa wananchi na serkali pamoja na wadau wengine kwakuwa ujenzi wa shule unahitaji nguvu kazi,raslimali fedha,pamoja mamlaka husika.
Kwaupande wake diwani wa ata ya isapulano ametoa pongezi zadhati kwa prof sigara kwa mchango wake wa fedha kiasi cha million moja kwaajili ya saruji kumalizia umaliziaji wa maabara na mabati 150 pamoja na juhudi za kuhakikisha shule inapewa usajili.
Aidha wananchi wa kata ya Isapulano wamemshukuru Mh.Mbunge kwa mchango wake huku wakirudisha matumaini ya kuondoka katika adha ya kusafiri umbali mrefu kupeleka watoto shule ambapo kwasasa wana safili zaidi ya kilometa mpaka 20 kupeleka watoto shule.


Share this article :

0 comments:

Post a Comment

 
Support : Copyright © 2018. AFRICAN NEWS BLOG - All Rights Reserved
Imetengenezwa na Edwin Moshi
Inaendeshwa na AFRICAN NEWS BLOG