Home » » MBUNGE AWASUUZA MIOYO WAKAZI WA KATA YA ISAPULANO

MBUNGE AWASUUZA MIOYO WAKAZI WA KATA YA ISAPULANO

Unknown | Friday, December 29, 2017 | 0 comments



Baadhi ya wazazi na walezi wa kata  ya isaplano wilayani makete mkoani njombe wamesema kuwa kuna umuhimu mkubwa wa kuwapeleka watoto shuleni kwani ni haki ya mtoto kisheria huku wakitoa wito kwa wazazi wengine kuwapeleka watoto shule ili kuongeza watalamu mbalimbali hapa nchini.
Wakizungumza na  AM BLOG wananchi hao wamesema kuwa kumpeleka mtoto shule kuna mjengea uwezo wa kutambua fursa mbalimbali za kimaendeleo ili kuwa na taifa ambalo lina wasomi wengi ambao wataleta chachu ya maendeleo katika taifa
Katika hatua nyingine wananchi hao wameiomba serikali kuchukua hatuka kali za kisheria kwa wazazi ambao hawata wapeleka watoto shule ili iwefundisho kwa wengine kwani kuna baadhi ya wazazi huwa hawataki kuwapeleka watoto shule kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo changamoto za kiuchumi.
WAKATI HUO HUO
Kutokana na changamoto ya ubovu wa barabara ya kutoaka luvulunge mpka isaplano wananchi wa kata ya isaplano wamesema barabara hiyo inakwamisha shughuli mbalimbali za kimaendeleo katani hapo ikiwemo kushindwa kusafirisha mazao yao kwa ajiri ya biashara jambo ambalo linapelekea wananchi na kushindwa kujikimu kataka maisha.




Share this article :

0 comments:

Post a Comment

 
Support : Copyright © 2018. AFRICAN NEWS BLOG - All Rights Reserved
Imetengenezwa na Edwin Moshi
Inaendeshwa na AFRICAN NEWS BLOG