Home » » Waziri Ataka Watoto Walioungana Kagera Wafikishwe Muhimbili Haraka

Waziri Ataka Watoto Walioungana Kagera Wafikishwe Muhimbili Haraka

Unknown | Tuesday, June 05, 2018 | 0 comments
Waziri wa Afya, Ustawi wa Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto , Ummy Mwalimu amemwagiza Mganga Mkuu wa Mkoa wa Kagera, kuhakikisha watoto waliozaliwa wakiwa wameungana wanafikishwa Muhimbili.

Waziri Ummy ametoa kauli hiyo leo bungeni wakati akijibu swali la nyongeza la Mbunge wa Viti Maalumu, Suzan Lyimo ambaye alihoji je serikali ina taarifa kuwa kuna watoto wamezaliwa Kagera wakiwa wameungana.

Akijibu swali hilo, Ummy amesema: “Wanaozaliwa wakiwa na maumbile ya ajabu wapelekwe hospitali.

“Na kuhusu watoto waliozaliwa wakiwa wameungana huko Kagera, namwagiza Mganga Mkuu wa Mkoa wa Kagera ahakikishe watoto hao wanafikishwa Muhimbili,”.

Advertisement
Share this article :

0 comments:

Post a Comment

 
Support : Copyright © 2018. AFRICAN NEWS BLOG - All Rights Reserved
Imetengenezwa na Edwin Moshi
Inaendeshwa na AFRICAN NEWS BLOG