Home » » Ommy Dimpoz- Sijawahi kutoka kimapenzi na Wema Sepetu......ile Ilikuwa ni Kiki Tu

Ommy Dimpoz- Sijawahi kutoka kimapenzi na Wema Sepetu......ile Ilikuwa ni Kiki Tu

Unknown | Saturday, May 05, 2018 | 0 comments
Mwanamuziki wa Bongo fleva Omari Nyembo maarufu kama Ommy Dimpoz amefunguka na kuweka wazi kuwa hajawahi hata siku moja kutoka kimapenzi na Wema Sepetu.

Kipindi cha nyuma ilishawahi kusemekana Kuwa Ommy Dimpoz na Wema Sepetu walikuwa kwenye mahusiano ya kimapenzi hasa baada ya picha zao kusambaa Kwenye mitandao ya kijamii.

Tetesi za Ommy dimpoz na Wema kuwa kwenye mahusiano zilizidi pale ambapo alionekana na Wema Kwenye chumbani wakiwa wamelala ambapo baadae ilikuja kujulikana walikuwa location kwa ajili ya kushoot wimbo wa Wanjera ambao Wema alikuwa ni video queen.

Lakini Kwenye mahojiano na Kipindi cha The Playlist cha Times Fm, Ommy Dimpoz amethibitisha kuwa zile zilikuwa ni kiki tu kwa ajili ya project zao.

"No, Sijawahi ku-date na msichana yeyote maarufu hapa Bongo, sijawahi.“

Lakini pia Ommy Dimpoz amesisitiza kuwa hajawahi kuwa na Mahusiano na msichana yoyote ambaye ni staa kwa Bongo.

Hivi sasa Ommy Dimpoz anafanya vizuri sana na wimbo wake wa Yanje aliomshirikisha Msanii Seyi Shay kutoka Nigeria.

Advertisement
Share this article :

0 comments:

Post a Comment

 
Support : Copyright © 2018. AFRICAN NEWS BLOG - All Rights Reserved
Imetengenezwa na Edwin Moshi
Inaendeshwa na AFRICAN NEWS BLOG