Home » » MAMILIONI YA FEDHA OKOLEWA NA TAKUKURU MKOA WA NJOMBE

MAMILIONI YA FEDHA OKOLEWA NA TAKUKURU MKOA WA NJOMBE

Unknown | Tuesday, May 15, 2018 | 0 comments

Image result for PICHA ZA PCCB
Taasisi ya kuzuia na Kupambana na Rushwa TAKUKURU Mkoa wa Njombe imeokoa kiasi cha Shilingi Milioni kumi na moja zilizokuwa zitumike tofauti na Matarajio kwenye Ujenzi wa Zahanati ya Itambo Wilayani Wanging’ombe

Kamanda wa TAKUKURU Mkoa wa Njombe CHARLES NAKEMBETWA akizungumza na Waandishi wa Habari ofisini kwake hii leo amesema mradi huo uliofadhiliwa na Ubalozi wa JAPAN kwa mwaka wa fedha 2011/2012 na kutengewa fedha zaidi ya Milioni mia saba ulioratibiwa na kusimamiwa na NG’O ya MSETI DEVELOPMENT ASSOCIATION ya Mjini Njombe

Hata hivyo pamoja na kulipwa fedha zote Kamanda huyo amesema kampuni hiyo haikuweza kukamilisha mradi huo kwa wakati  hivyo TAKUKURU baada ya kupata taarifa ilianza kufanya uchunguzi na kubaini tatizo kwenye mradi huo

Pia afisa huyo wa TAKUKURU amesema fedha hizo zilizookolewa zitakabidhiwa katika ofisi ya Katibu Tawala Mkoa wa Njombe aliyekuwa Msimamizi wa Mradi huo ili ziweze kufanya kazi ya ujenzi wa Zahanati husika
Na uchunguzi utakapokamilika wahusika watafikishwa Mahakamani

Share this article :

0 comments:

Post a Comment

 
Support : Copyright © 2018. AFRICAN NEWS BLOG - All Rights Reserved
Imetengenezwa na Edwin Moshi
Inaendeshwa na AFRICAN NEWS BLOG