Home » » Wanafunzi Shule ya Msingi Luvulunge wameanza kunufaika na Elimu ya wasaidizi wa Kisheria

Wanafunzi Shule ya Msingi Luvulunge wameanza kunufaika na Elimu ya wasaidizi wa Kisheria

Unknown | Tuesday, May 15, 2018 | 0 comments

Image result for PICHA ZA SHULE
Wanafunzi Shule ya Msingi Luvulunge iliyopo kata ya Isapulano Wilayani Makete wameanza kunufaika na Elimu ya wasaidizi wa Kisheria inayotolewa na Shirika la Makete Paralegal Organisation(MAPAO)

Mkurugenzi wa Shirika hilo la Wasaidizi wa Kisheria Wilaya ya Makete DENIS SINENE amesema utoaji wa Elimu hiyo kwa Wanafunzi ni katika kuwasaidia watoto kuwa na Misingi bora ya Elimu na kujua haki zao za Msingi ikiwa ni pamoja na wao kutambua wajibu wao

Mkurugenzi wa Shirika hilo la Wasaidizi wa Kisheria Wilaya ya Makete DENIS SINENE Ametoa Maelezo hayo wakati wa kuanzisha Klabu ya Wasaidizi Shuleni hapo ikiwa ni Mwendelezo wa kuanzisha Klabu hizo kwenye Shule za Sekondari na Msingi Wilayani hapa

Mkurugenzi huyo ameelezea dhamira na Lengo la kuwepo kwa Wasaidizi wa Kisheria Wilayani hapa pamoja na kuwataka watoto kuwa watiifu kwa wazazi wao na Jamii inayowazunguka

Kwa Upande wake Mjumbe wa Bodi ya MAPAO amesema wanafunzi hao wakiendelea kupatiwa Elimu hiyo mara kwa mara Taifa litakuja kuwa na Vijana waadilifu na kuyaishi mema wakati wote

Mkurugenzi wa Shirika hilo la Wasaidizi wa Kisheria Wilaya ya Makete DENIS SINENE amesema watoto wanatakiwa kujitambua kwa kujua wajibu wao kwa wazazi huku Klabu ya wasaidizi wa Kisheria iliyoundwa hii leo shuleni hapo ikiwa na wajumbe Zaidi ya 40
Shirika la Wasaidizi wa Kisheria Wilaya ya Makete MAPAO linaanzisha Klabu 2 za Wasaidizi wa Kisheria kwa Wanafunzi moja kutoka shule ya Sekondari Iwawa na Klabu nyingine imeanzishwa leo shule ya Msingi Luvulunge na leo ni kuendelea kutoa Elimu ya Kisheria kwa wanafunzi shule zote za Msingi na Sekondari Wilayani hapa

Share this article :

0 comments:

Post a Comment

 
Support : Copyright © 2018. AFRICAN NEWS BLOG - All Rights Reserved
Imetengenezwa na Edwin Moshi
Inaendeshwa na AFRICAN NEWS BLOG