Home » » Amber Lulu: Sina mpango wa mtoto kwa sasa

Amber Lulu: Sina mpango wa mtoto kwa sasa

Unknown | Saturday, April 28, 2018 | 0 comments
Msanii wa muziki Bongo na Video Vixen, Amber Lulu amefunguka mipango yake ya kuitwa mama.

Muimbaji huyo anayefanya vizuri na ngoma ‘Jini Kisirani’ ameiambia XXL ya Clouds FM kuwa bado anajipanga kwa ajili ya suala hilo ila kwa sasa hana mpango.

“Kwa kweli kwa sasa hivi sijatarajia bado, vitu vyangu vingi bado sijakamilisha,” amesema.

“Sio Gigy Money amepata mtoto na mimi nipate, no! unajua unapopata mtoto kuwe na maandalizi yake. Labda yeye rafiki yangu kajiandaa mtoto lazima aje kwenye mazingira mazuri,” ameongeza.

Gigy Money ambaye yupo katika mahusiano na Mtangazaji wa Choice FM, M o J alijifungua mtoto wa kike usiku wa kuamkia jana April 27, 2017 na amempa mwanae jina Mayra.
Share this article :

0 comments:

Post a Comment

 
Support : Copyright © 2018. AFRICAN NEWS BLOG - All Rights Reserved
Imetengenezwa na Edwin Moshi
Inaendeshwa na AFRICAN NEWS BLOG