Home » » WANANCHI WAKATAA KUPOKEA MRADI,MWENYEKITI WA KAMATI AGOMA KUFANYA UCHUNGUZI,DIWANI ATOA SIKU SABA

WANANCHI WAKATAA KUPOKEA MRADI,MWENYEKITI WA KAMATI AGOMA KUFANYA UCHUNGUZI,DIWANI ATOA SIKU SABA

Unknown | Wednesday, February 07, 2018 | 0 comments
  Tokeo la picha la wananchi ukwama makete
Na Bonfasi Mwafulilwa.
wananchi wa kijiji cha Ihanga kata ya Ukwama wilayani makete mkoani njombe wamelaani vikali kitendo cha kamati ya kijiji hicho kutumia fedha za ujenzi wa choo cha wanafunzi katika shule ya msingi Ihanga kutumia katika miradi mingine hali iliyopelekea kusimama kwa ujenzi wa choo hicho.

hayo yamejitokeza hii leo february 7,2018 katika kikao cha serikali ya kijiji cha Ihanga wilayani Makete Mkoani Njombe kilicholenga kujadili mambo mbali mbali likiwemo suala la sababu zilizopelekea kusimama kwa ujenzi wa choo cha wanafunzi katika shule ya msingi Ihanga.

mwenyekiti wa kijiji hicho Juma Ndelwa akisoma taarifa ya matumizi ya  fedha shilingi milioni tano ambazo zilitengwa kwa ajili ya ujenzi wa choo cha wanafunzi shuleni hapo,ambayo kwa mujibu wa mwenyekiti huyo pesa hiyo imetumika katika shughuli mbali mbali ya shule ikiwemo kununua miche ya parachichi za kupanda shuleni hapo.
miche ya parachichi za kupanda shuleni hapo.
kufuatia maelezo hayo wananchi wa kijiji cha Ihanga kata ya Ukwama hawakupendezwa na maelezo hayo kwa kwa kuwa mipango ya pesa hizo ilikuwa kujengea choo cha wanafunzi shuleni.
Kutokana na kujitokeza kwa hali ya wananchi kutokuwa na imani na suala hilo mh, diwani wa kata hiyo Agustino Tweve akamwagiza mwenyekiti wa kamati ya shule kukaa na kamati yake ili waweze kulifuatilia suala hilo huku akitoa siku saba za kufanya uchunguzi huo.
kwaupande wake mwenyekiti wa kamati ya shule hiyo Philipo Sanga amegoma kufanya jambo hilo huku akidai hatua zozote zitakazochukuliwa dhidi yake yuko tayari kuupokea.
Mheshimia diwani Tweve baada ya kusikia kuwa mwenyekiti wa kamamti ya shule bwana Philipo Sanga kukaidi agizo lake amesema sheria kali itachukuliwa endapo ataona utekelezaji wa sula hilo ambalo linalalamikiwa na wananchi halitafanikiwa.
Share this article :

0 comments:

Post a Comment

 
Support : Copyright © 2018. AFRICAN NEWS BLOG - All Rights Reserved
Imetengenezwa na Edwin Moshi
Inaendeshwa na AFRICAN NEWS BLOG