Baadhi ya wananchi wakiwa nje ya Nyumba hiyo baada ya kuuzima moto huo
Baadhi ya vitu vilivyokuwemo ndani vikionekana baada ya kutolewa nje
Na Furahisha Nundu
Matukio ya nyumba kuungua yamezidi
kushamiri Mji mdogo wa Iwawa hususani Kitongoji cha Dombwela Wilayani
Makete baada ya nyumba nyingine kuungua hii leo na chanzo chake
kikidaiwa kuwa huenda ni Shoti ya Umeme
Tukio la kuungua kwa Nyumba ya Mwanamke
mmoja Aliyetambulika kwa Jina la Agatha limesababisha Samani mbalimbali
kuteketea kwa moto huo ikiwemo Sofa na vifaa vingine ambavyo bado
thamani yake haijajulikana
Mama anayeishi kwenye nyumba hiyo
Kitongoji cha Dombwela karibu na Msikitini ambaye hakuwepo wakati tukio
hilo linatokea amesema "Nilikuwa Kanisani nimeondoka hapa nyumbani saa
nne kasoro na hapakuwa na mtu ghafla nikiwa Kanisani nikaja kuambiwa
nyumbani kuna tatizo nirudi lakini nafika nyumbani nakuta watu wamejaa
nje ya nyumba na vyombo vyote vikiwa nje hapa".
"Sijui chanzo cha moto huu ni nini
lakini kusema ni Jiko la Mkaa hapana mimi sijawahi kutumia jiko hilo
natumia kuni,Lakini kwa kweli nawashukuru Majirani na watu wote
waliozima moto huu Mungu awabariki sana" Alisema Agatha.
Agnes Sanga ni jirani yake na Agatha
yeye alikuwa shuhuda wa kwanza kufika eneo la tukio amesema alipoona
nyumba inatoa moshi alipiga simu kwa watu wengine na kuwaita majirani na
kuanza kubomoa Milango na Madirisha ndipo wakaona moto unawaka ndani ya
Sebule na kuanza kuuzima kwa kutumia Maji.
Ameongeza kuwa watu walikusanyika Haraka
na kuanza kusaidia kuzima moto huo jambo ambalo walifanikiwa kwa kiasi
fulani kuokoa mali zilizokuwemo ndani,huku akisema moto huo unaonekana
ulianzia juu ya Dari Sebuleni.
Mwenyekiti wa Kitongoji cha Dombwela
Ndg.Joseph Mbilinyi amesema kwamba anasikitishwa na tukio hilo huku
akiwashukuru wananchi waliojitokeza kwa wingi kuuzima moto huo na kuokoa
mali zilizokuwepo ndani ya nyumba hiyo
Hili ni tukio la tatu kutokea kwa kipindi cha miezi Isiyozidi mitano katika Kitongoji hicho cha Dombwela Mji mdogo wa Iwawa
0 comments:
Post a Comment