Serikali Mkoni Njombe imeombwa kutoa
misaada kwa wahanga wanao ishi katika mazingira magumu na hatarishi ili
kunusuru maisha yao kwani wamekuwa wanashindwa kukidhi mahitaji muhimu
katika familia zao ikiwemo chakula na malazi
Ni katika hali isiyo ya kawaida kwa
mtoto James Ndelwa mwenye umri wa miaka 16 mkazi wa mtaa wa Kihesa
Halmashauri ya Mji Njombe Mkoani Njombe amekuwa anasumbuliwa na ugojwa
usio julika, huku vipimo kutoka kwa madaktari vikionesha kuto kuwepo kwa
ugonjwa wowote kama anavo eleza Felister Sanga ambae ni mama mzazi wa
mtoto huyo amesema kuwa zaidi ya miaka kumi mtoto wake huyo amekuwa
akisumbuliwa na ugonjwa Usiojulikana huku akiwa amezunguka kwenye vituo
mbalimbali vya afya bila mafanikio yoyote
Majirani ambao wamekuwa wanamsaidi mama
huyo katika kuhakikisha kwamba wanampa faraja na matumaini ya kuishi na
mtoto huyo wameiomba jamii pamoja na serikali na asasi mbalimbali mkoani
hapa kumpa msaada mama huyo ili kumwezesha mtoto huyo kupona kwani mama
mzazi wa mtoto huyo amekuwa anashinda bila kufanya kazi inayo weza
kumwingizia kipato kwa kushinda anamwangalia mtoto huyo.
Jesca Sanga ambaye ni Jirani na Mama
James anasema "Kwa kweli huyu jirani yangu namunea huruma sana jinsi
anavyonyanyasika na huyu mtoto ameteseka kwa siku nyingi sana,kwa sababu
hata mama mwenyewe anashindwa hata kufanya kazi tunashindwa hata
kuelewa huyu mtoto anatatizo gani yaani"
0 comments:
Post a Comment