Home » » Mashambulizi Syria yasababisha raia kushindwa kupumua

Mashambulizi Syria yasababisha raia kushindwa kupumua

Unknown | Monday, February 05, 2018 | 0 comments



Raia kadhaa wa Syria wanatibiwa baada ya kushindwa kupumua kutokana na mashambulizi ya ndege yaliyofanywa na serikali kwenye mji wa Saraqeb. 

Shirika linalofuatilia haki za binaadamu nchini Syria lenye makao yake mjini London, Uingereza limesema raia watano wanapatiwa matibabu kutokana na kukosa pumzi na kushindwa kupumua baada ya serikali ya Syria kutumia silaha za sumu katika maeneo yanayodhibitiwa na waasi kwenye mji wa Saraqeb uliopo kaskazini magharibi mwa Syria.

Duru za kitabibu zimeeleza kuwa wagonjwa wengine 11 walikuwa wakitibiwa kutokana na gesi yenye sumu ya Chlorine, iliyotumika katika shambulizi hilo. Shambulizi hilo limefanyika siku chache baada ya Marekani kuishutumu serikali ya Syria kwa kutumia silaha za kemikali dhidi ya vikosi vya waasi karibu na mji mkuu, Damascus.

Hata hivyo serikali ya Syria imekanusha madai hayo ikiyaita kuwa ni ''uongo''. Siku ya Ijumaa Waziri wa Ulinzi wa Marekani, Jim Mattis aliwaambia waandishi habari kwamba serikali yake ina wasiwasi gesi ya sarin huenda ikawa imetumika hivi karibuni nchini Syria, ikizinukuu taarifa za mashirika yasiyokuwa ya kiserikali pamoja na makundi ya waasi.

Share this article :

0 comments:

Post a Comment

 
Support : Copyright © 2018. AFRICAN NEWS BLOG - All Rights Reserved
Imetengenezwa na Edwin Moshi
Inaendeshwa na AFRICAN NEWS BLOG