Home » » Israel kuanza kuwatimua wahamiaji wa Kiafrika

Israel kuanza kuwatimua wahamiaji wa Kiafrika

Unknown | Monday, February 05, 2018 | 0 comments

Israei yatoa ilani kwa maelfu ya wahamiaji wa kiafrika ikiwataka waondoke kufikia mwezi Machi. Maafisa wanasema kwamba endapo onyo hilo halitotekelezwa wahamiaji huenda wakajikuta wakikamatwa na kufungwa jela.

Wakimbizi wakiafrika walipoandamana Jerusalem 17.01.2018
Israel imeanza kutoa onyo kwa maelfu ya wahamiaji wa kiafrika tangu hapo jana ikiwataka waondoke nchini humo kufikia mwezi Machi. Maafisa wanasema kwamba endapo onyo hilo halitotekelezwa wahamiaji huenda wakajikuta wakikamatwa na kufungwa jela.

Maafisa nchini Israeli wameshaanza hatua ya kugawa vikaratasi vya ilani kwa wahamiaji wa kiafrika kuanzia hapo jana wakitakiwa kufunganya virago kwa khiari na kuiaga nchi hiyo chini ya mpango maalum unaolenga kuwaondowa kiasi watu 38 elfu wanaoomba hifadhi katika taifa hilo la Mashariki ya Kati, amesema msemaji wa wizara ya mambo ya ndani ya Israel.

Ilani hiyo inayotowa muda wa miezi miwili  kwa wahamiaji kuondoka inatajwa kwamba inatolewa kwa wanaume wasiokuwa na watoto. Serikali ya Israel inawataja waomba hifadhi walioko nchi humo  kuwa ni wahamiaji wanaotafuta maslahi ya kiuchumi ikiwaita kwamba ni watu waliojipenyeza nchini humo.
Hivi karibuni waziri mkuu Netanyahu alisikika akisema:   


Waziri mkuu Netanyahu akiwa Uganda na rais Museveni Julai 2017
Kwa mujibu wa mpango wa Israel wahamiaji watakaoamua kuchagua kuondoka kwa khiari watapewa dolla 3,500 pamoja na tiketi ya ndege  ya kwenda nchi nyingine ambayo haikutajwa. Wanawake ,watoto na kina baba wanaotegemewa na watoto wao hawaguswi katika mpango huo. Hata hivyo kuanzia mwezi Aprili kiwango cha dolla 3500 zinazotolewa kitapunguzwa taratibu na endapo kuna mhamiaji aliyeamua kubakia katika nchi  hiyo atakuwa katika uwezekano wa kufungwa
Share this article :

0 comments:

Post a Comment

 
Support : Copyright © 2018. AFRICAN NEWS BLOG - All Rights Reserved
Imetengenezwa na Edwin Moshi
Inaendeshwa na AFRICAN NEWS BLOG