Home » » Kamanda Sirro aitaka jamii kushirikiana na Polisi kutokomeza makosa ya kihalifu

Kamanda Sirro aitaka jamii kushirikiana na Polisi kutokomeza makosa ya kihalifu

Unknown | Friday, February 02, 2018 | 0 comments

Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Simon Sirro ameitaka jamii pamoja viongozi wa dini kushirikiana na Polisi ili kutokomeza makosa mbalimbali katika jamii ikiwemo mauaji yatokanayo na wivu wa mapenzi, ulevi, ubakaji ili kuiweka nchi salama zaidi.
IGP Sirro ameeleza hayo leo Jijini Dar es Salaam ambapo amesema kuwa takwimu za sasa zinaonyesha matukio ya aina hiyo yamekithiri sana nchini Tanzania jambo ambalo jamii inapaswa kubadilika ili kupunguza matukio hayo.
“Kuna makosa ambayo watu lazima wabadilike na hili haliitaji Jeshi la Polisi maana mimi nasimamia  Sheria lakini kuna viongozi wa dini wazungumzie hayo mambo. Muumini wako akija Kanisani au Msikiti na ukimwambia katazo la Mungu anaweza akabadilika”,.
Kwa upande mwingine, Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Sirro amesema kuna makosa ambayo viongozi wa dini wakishiriki kwa ukaribu zaidi inaweza kupunguza huku akiitaka jamii kubadilika kitabia ikiwemo kuachana na ulevi wa kupindukia.
Share this article :

0 comments:

Post a Comment

 
Support : Copyright © 2018. AFRICAN NEWS BLOG - All Rights Reserved
Imetengenezwa na Edwin Moshi
Inaendeshwa na AFRICAN NEWS BLOG