Home » » Chadema Walimwa Barua.....wadaiwa kukiuka maadili ya uchaguzi Kinondoni

Chadema Walimwa Barua.....wadaiwa kukiuka maadili ya uchaguzi Kinondoni

Unknown | Thursday, February 01, 2018 | 0 comments
Wakati kampeni za uchaguzi jimbo la Kinondoni zikiendelea, Chadema wamepewa barua mbili za malalamiko na  msimamizi  wa uchaguzi Wilaya ya Kinondoni, Aron Kagurumjuli kikidaiwa kuvunja kanuni za maadili ya uchaguzi.

Akizungumza leo Februari 1, 2018 Mkurugenzi  wa Operesheni na Mafunzo wa Chadema, Benson Kigaila amesema wamepokea barua hiyo jana, yenye malalamiko yaliyotolewa na Chama cha Wananchi (CUF).

Katika barua hiyo, CUF inalalamika kuwa Januari 28, Chadema walifanya kampeni nyumba kwa nyumba  katika eneo la Kigogo Mbuyuni hadi London Bar badala ya siku hiyo kuwa kata ya Ndugumbi kama ratiba inavyoonyesha.

Malalamiko mengine ni Chadema kudaiwa kutumia salama ya CUF katika majukwaa ya kampeni sambamba na kupamba bendera za chama hicho.

"Madai mengine ni kwamba viongozi  wa CUF  wanakuja katika mikutano yetu  na kukaa meza kuu na kupanda katika majukwaa. Pia CUF wanadai Chadema inawatumia viongozi  wao kupita nyumba kwa nyumba kuiombea kura Chadema  wakiwa na sare za CUF,” amesema Kigaila.

Kwa mujibu wa barua hizo Chadema wanatakiwa kutoa maelezo ya utetezi kwa maandishi  kuhusu tuhuma hizo ndani ya saa 48 baada ya kuzipokea.

Advertisement
==
Share this article :

0 comments:

Post a Comment

 
Support : Copyright © 2018. AFRICAN NEWS BLOG - All Rights Reserved
Imetengenezwa na Edwin Moshi
Inaendeshwa na AFRICAN NEWS BLOG