Home » » Mwanamuziki wa Nyimbo za Injili nchini Tanzania Matha Baraka atoa siri nzito ya kufanikiwa kimuziki .

Mwanamuziki wa Nyimbo za Injili nchini Tanzania Matha Baraka atoa siri nzito ya kufanikiwa kimuziki .

Unknown | Saturday, January 06, 2018 | 0 comments



Mwanamuziki wa Nyimbo za Injili nchini Tanzania Matha Baraka atoa siri nzito ya kufanikiwa kimuziki huku akitoa wito kwa waimbaji wa nyimbo za Injili kumtumikia Mungu kwa waminifu hali wakijua kuwa waimbaji wana hubiri Neno kupitia Wimbaji.

Matha Baraka amesema kuwa siri kubwa ni wokovu na kuishi kwa kumtegemea Mungu,ameyasema hayo alipokuwa akizungumza na AFRICAN NEWS BLOG huku akisema mafanikio hayo yametokana na kumtumikia Mungu kwa waminifu na bidii.

Aidha amesema kwa mwaka 2018 amejipanga zaidi katika kufanya Injili ndani na nje ya mipaka ya Tanzania ambapo amesema kwa mwaka 2017 amemwona Mungu akimtumia katika viwango Vya juu zaidi ambapo muda mwingi amekuwa akihudumia maelfu ya watu katika maeneo tofauti.

Katika hatua nyingine Bi, Matha Baraka,ametoa wito kwa waimbaji kutoimba kwa mazoeya na kuimba kwa kusikia sauti ya kristo kuliko kuiga mafuta (uimbaji) ya wengine ambapo amesema kila mwimbaji ana ujumbe ambao Mungu amempa kwaajili ya watu wake.

Kwa sasa Matha Baraka anatamba na Albamu ya Nimekuja na Maua una weza kuitazama kupitia Yotube,na mitandao mingine ya kijamii.



Share this article :

0 comments:

Post a Comment

 
Support : Copyright © 2018. AFRICAN NEWS BLOG - All Rights Reserved
Imetengenezwa na Edwin Moshi
Inaendeshwa na AFRICAN NEWS BLOG