Home » » Msemaji Mkuu wa Serikali amemjibu Tundu Lissu

Msemaji Mkuu wa Serikali amemjibu Tundu Lissu

Unknown | Friday, January 05, 2018 | 0 comments
Mkurugenzi Mkuu-Idara ya Habari, Maelezo na Msemaji Mkuu, Dkt Hassan Abbas amesem kwamba Tundu Lissu bado ni mgonjwa na yuko wodini hivyo Serikali haioni busara kulumbana naye kwa sasa.

Dkt Abbasi ameeleza kuwa, kwa sasa serikali bado inaendelea kumuombea mbunge huyo ili aweze kupona haraka.

Maneno hayo yametolewa ikiwa ni mida mfupi tangu Tundu Lissu ambaye ni Mbunge wa Singida Mashariki alipozungumza na waandushi wa habari akiwa Hospitalini jijini Nairobi na kuituhuma serikali kuhusu masuala mbalimbali ya ukiukwaji wa haki za binadamu.

Miongoni mwa mambo mengi ambayo Tundu Lissu ameituhumu serikali ni pamoja na jaribio la kutaka kumuua lililotokea Septemba 7 mjini Dodoma, ambapo Lissu amesema licha ya kuwa miezi minne imepita tangu aliposhambuliwa kwa lengo la kuuawa, hakuna kiongozi yoyote wa serikali aliyekemea tukio hilo.

Lissu ameelekeza malalamiko yake pia kwa Bunge ambapo amekosoa uamuzi wa Bunge kukataa kugharamia matibabu yake, na kuacha mzigo wote kwa chama na familia.

Advertisement
==
Share this article :

0 comments:

Post a Comment

 
Support : Copyright © 2018. AFRICAN NEWS BLOG - All Rights Reserved
Imetengenezwa na Edwin Moshi
Inaendeshwa na AFRICAN NEWS BLOG