Home » » Hatari yainyemelea Lupalilo Sekondari, Umeme haupo mwezi mzima sasa

Hatari yainyemelea Lupalilo Sekondari, Umeme haupo mwezi mzima sasa

Unknown | Thursday, January 18, 2018 | 0 comments

 Transfoma iliyopata tatizo
Shule ya sekondari ya Lupalilo  inakabiliwa na ukosefu wa nishati ya umeme kwa zaidi ya mwezi mmoja hivi sasa baada ya Transfoma iliyokuwepo kuungua na kusababisha kukwama kwa shughuli mbalimbali  shuleni hapo ikiwemo  wanafunzi kushindwa kujisomea usiku pamoja na   kuhatarisha usalama  wa wanafunzi baada  kukosekana kwa  nishati hiyo hasa nyakati za usiku
Akizungumzia Hali hiyo makamu mkuu wa shule Mwalimu LUNANILO KILATU amesema ni zaidi ya mwezi mmoja sasa  wamekosa nishati hiyo baada ya transfoma kuungua na kupelekea  baadhi ya shughuli kukwama shuleni hapo ikiwemo wanafunzi kushindwa kujisomea nyakati za usiku hivyo shule kulazimika kutumia jenereta ambalo amedai linawaongezea gharama zaidi
Amesema wamesharipoti suala hilo kwa shirika la umeme TANESCO wilaya ya Makete tangu lilipotokea lakini hadi sasa ufumbuzi haujapatikana ingawa anaimani kuwa wanashughulikia

Kwa upande wa baadhi ya wanafunzi shuleni hapo waliozungumza na mwandishi wetu wamesema wanakumbana na changamoto nyingi baada ya kukosekana nishati hiyo ikiwemo kushindwa kujisomea nyakati za usiku huku wakihofia juu ya usalama wao hususani wanafunzi wa kike

Hata hivyo Tumemtafuta Meneja wa Tanesco wilaya ya Makete Ndugu HENRIKO RENATUS  kupata ufafanuzi ambapo amesema mpaka sasa wanasubiri Transfoma nyingine kwani wameshatuma maombi ya kuomba transfoma na pindi zitakapowasili wataipa kipaumbele shule hiyo kutokana na uhitaji


Ni zaidi ya mwezi sasa shule hiyo ikabiliwa na tatizo hilo la ukosefu wa umeme na kukwamisha mambo mengi pamoja na usalama wa wanafunzi kuwa mdogo na kupunguza uwezekano  wa wanafunzi kujisomea nyakati za usiku kama ilivyokuwa awali

Makamu Mkuu wa shule akizungumza na mwandishi wetu ofisini kwake
 Mwanafunzi wa Lupalilo Sekondari akizungumza na mwandishi wetu
 Muonekano wa shule ya Lupalilo Sekondari
Share this article :

0 comments:

Post a Comment

 
Support : Copyright © 2018. AFRICAN NEWS BLOG - All Rights Reserved
Imetengenezwa na Edwin Moshi
Inaendeshwa na AFRICAN NEWS BLOG