Home » » WANANCHI MAKETE WATAKIWA KUJITOKEZA KUPIMA VVU NA UKIMWI ILIKUENDELEA KUPUNGUZA MAAMBUKIZI MAPYA

WANANCHI MAKETE WATAKIWA KUJITOKEZA KUPIMA VVU NA UKIMWI ILIKUENDELEA KUPUNGUZA MAAMBUKIZI MAPYA

Unknown | Wednesday, December 27, 2017 | 0 comments


Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Makete Ndugu Francis Namaumbo amwewaomba wananchi wilayani makete kujitokeza kupima maambikizi ya virusi vya Ukimwi ili kupunguza ongezeko la maambukizi mapya ya  VVU katika wilaya ya Makete mkoani Njombe.

Rai hiyo ameitoa hapo jana  katika Tamasha la Nguvu ya Mwaka 2017 lililoandaliwa na kitulo Fm Radio  ambalo lililofanyaka  ukumbi wa madihani Villas Lodge.

Namaumbo ameongeza kuwa kutokana na wilaya ya makete kuwa na ongezeko kubwa la virusi vya ukimmwi amewaomba vijana pamoja na wananchi kwa ujumla kujitokeza kupima ili kujua afya zao.

Mkurugenzi wa Madihani Villas Lodge Abel Mbilinyi ameipongeza Kitulo Fm Redio kwa kuandaa Tamasha hilo la kutoa Elimu kwa Vijana kuhusu Fursa mbalimbali za kiuchumi na Wadau wote waliofika Ukumbini hapo

Kitulo fm Radio iliandaa Tamasha la nguvu ya mwaka 2017 kwa lengo la kupunguza maambukizi ya virusi vya ukimwi,kutoa elimu kwa vijana kuhusu fursa za ujasiriamali,kutoa elimu kwa wananchi kuhusu ukatili kwa watoto,kutoa elimu kuhusu kutokomeza rushwa katika wilaya ya makete.

Mratibu wa Tamasha la nguvu ya mwaka Aldo sanga kwa kushirikiana wafanya kazi wa kitulo fm radio wamewashukuru wadau wote waliohudhurua kwenye tamasha hilo.

Share this article :

0 comments:

Post a Comment

 
Support : Copyright © 2018. AFRICAN NEWS BLOG - All Rights Reserved
Imetengenezwa na Edwin Moshi
Inaendeshwa na AFRICAN NEWS BLOG