Home » » Mtumishi wa umma akamatwa na dawa za kulevya kg 216.3

Mtumishi wa umma akamatwa na dawa za kulevya kg 216.3

Unknown | Thursday, December 28, 2017 | 0 comments
Jeshi la Polisi Mkoa wa Kilimanjaro linamshikilia mfanyakazi wa kike wa Mfuko wa Pensheni wa Mashirika ya Umma (PPF) kwa tuhuma za kukutwa na dawa za kulevya aina ya bangi ndani ya gari lake.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro, Hamis Issa, amesema kwamba mtuhumiwa huyo ambaye ni mkazi wa Karanga katika Halmashauri ya Manisapaa ya Moshi, alikamatwa akiwa na kilogramu 216.3 za bangi ndani ya gari lake aina ya Toyota Sienta.
Mtuhumiwa huyo alikamatwa eneo la Majengo kwa Mtei, Disemba 19 alipokuwa  njiani akitokea Himo.
Kamanda Issa amesema kuwa, biashara ya bangi inabaki kuwa changamoto kubwa sana katika mikoa ya kaskazini, na kwamba jeshi la polisi linafanyakazi kwa jitihada zote kuhakikisha linatokomeza hali hiyo.
Aidha, alionesha masikitiko yake kufuatia watumishi wa umma ambao ndio walitakiwa kuwa mstari wa mbele kupiga vita dawa za kulevya, wakijihusisha kwenye biashara hiyo.
Share this article :

0 comments:

Post a Comment

 
Support : Copyright © 2018. AFRICAN NEWS BLOG - All Rights Reserved
Imetengenezwa na Edwin Moshi
Inaendeshwa na AFRICAN NEWS BLOG