Home » » Breaking News: Mwanafunzi apigwa Shoti ya Umeme na Kufariki akianika Nguo

Breaking News: Mwanafunzi apigwa Shoti ya Umeme na Kufariki akianika Nguo

Unknown | Wednesday, December 27, 2017 | 0 comments
Mwanafunzi wa kidato cha pili katika shule ya sekondari Enhencement Center iliyopo mkoani Njombe, aliyefahamika kwa jina moja la HOSSANA amefariki dunia baada ya kupigwa na shoti ya umeme wakati akianika nguo kwenye kamba ya waya.

Tukio hilo limetokea mtaa wa Kambarage Mkoani Njombe ambapo kwa mujibu wa shuhuda Daud Given Mwatija ambaye ni Afisa magereza amesema katika mtaa wao ni kweli mwanafunzi huyo amefariki ambapo kulikuwa na waya unaopeleka umeme kwenye jengo walilokuwa wakiishi (familia ya mwanafunzi huyo) uliokuwa umechubuka na kugusa nyumba hiyo hali iliyopelekea jengo zima kuwa na umeme, lakini wakati mwanafunzi huyo akianika nguo kwenye kamba ya umeme hakujua kama waya huo nao ulikuwa ukipitisha umeme, akapigwa shoti na kufariki dunia

Tukio hilo limetokea jana
Share this article :

0 comments:

Post a Comment

 
Support : Copyright © 2018. AFRICAN NEWS BLOG - All Rights Reserved
Imetengenezwa na Edwin Moshi
Inaendeshwa na AFRICAN NEWS BLOG