Home » » Aliyemlawiti Mtoto kwa zaidi ya Mwaka mmoja atiwa mbaroni

Aliyemlawiti Mtoto kwa zaidi ya Mwaka mmoja atiwa mbaroni

Unknown | Wednesday, December 27, 2017 | 0 comments
Jeshi la Polisi Mkoa wa kipolisi Tarime/Rorya, linamshikilia Said Selemani 30-40 mkazi wa Mtaa wa Kebasa Halmashauri ya Mji Tarime mkoani Mara kwa tuhuma za kulawiti mtoto wa miaka minne.
Kamanda mkoa wa kipolisi Tarime/Rorya, Henery Mwaibambe, amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kusema mtuhumiwa  amefunguliwa shtaka kituoni hapo namba TAR/IR/5034/2017 na kuwa atafikishwa mahakamani baada ya upelelezi kukamilika.
Aidha, Kamanda huyo aliongeza kuwa mtuhumiwa anatarajiwa kupelekwa mahakamani kesho ili kujibu shtaka linalomkabili ikiwa ni pamoja na kumsababishia maumivu makali mtoto huyo.
Akizungumzia tukio hilo nyumbani kwake, mama mzazi wa mtoto huyo (jina limehifadhiwa), amesema amelipokea kwa mshituko mkubwa tukio hilo ambapo lilibainika Disemba 14, 2017 wakati mtoto aliposhindwa kula na kuanza kuharisha mara kwa mara.
Kugundua kuwa mtoto wangu ameathirika na kitendo hicho ni baada ya kuwa ameshindwa kula huku akiwa anaharisha  mara kwa mara, kitendo ambacho kilinishtua  moyo wangu na mtoto hakuwa na dalili ya kuugua ikabidi nianze kufanya ufuatiliaji  wa kina ili kujua kilichompata,” alisema.
Ameongeza kuwa tukio hilo amelipokea kwa masikitiko makubwa na kuwa hakuwa na habari kuwa mwanaye wa miaka minne anaweza kutendewa kitendo cha kinyama kiasi hicho  na mtuhumiwa ambaye ni mpangaji mwenzake.
Akizidi kufafanua, amesema kuwa baada ya kugundua mwanaye amekuwa akilawitiwa mara nyingi kwa nyakati tofauti, alichukua hatua za kwenda kwa wataalamu ili kuchukuliwa vipimo kwa ajili ya kijiridhisha.
Hatua nilizochukua baada ya kugundulika kuwa mwanangu alikuwa ameathirika kwa muda mrefu ni kwenda kituoni polisi ili kutoa taarifa kwa  hatua zaidi kuchukuliwa dhidi ya mtuhumiwa,”alisema mama huyo..
Baada ya kwenda polisi ilibidi twende hospitalini kwa uchunguzi ambapo daktari alisema hakuona dalili zozote ila nikasema kuwa haiwezekani kuna mchezo unafanywa, andipo niliomba kwenda Bugando kwa uchunguzi zaidi ambapo polisi walitoa askari wa kwenda kujiridhisha,” aliongeza.
Alibainisha wakati wakiwa Bugando, daktari aliyemfanyia vipimo alisema mtoto huyo amelawitiwa mara nyingi zaidi ya mwaka mmoja.
Share this article :

0 comments:

Post a Comment

 
Support : Copyright © 2018. AFRICAN NEWS BLOG - All Rights Reserved
Imetengenezwa na Edwin Moshi
Inaendeshwa na AFRICAN NEWS BLOG