Home » » WANANCHI WA KATA YA ISAPULANO WATAKIWA KUTUNZA VITAMBULISHO VYA KUPIGIA KURA

WANANCHI WA KATA YA ISAPULANO WATAKIWA KUTUNZA VITAMBULISHO VYA KUPIGIA KURA

Unknown | Monday, April 09, 2018 | 0 comments
Image result for PICHA GREGORI EMMANUEL
Kufuatia aliyekuwa diwani wa kata ya isapulano bwana ALFONCE MBILINYI kujiuzulu kutoka chama cha demokrasia na maendeleo [CHEDEMA] kuhamia chama cha mapinduzi [CCM]Wananchi wa kata ya isapulano wilayani makete mkoani njombe wameaswa  kutunza vitambulisho vya kupigia kura kwa ajili ya uchaguzi wa marudio wa diwani wa kata hiyo.
Afisa uchaguzi wa wilaya ya makete bwana GREGORY EMANUEL amesema kuwa vitambulisho hivyo vitasaidia kupiga kura ili kuweza kumchagua diwani mwingine kutokana na diwani wa awali kujiuzulu na kuhamia chama kingine na kuacha nafasi hiyo wazi.

Wakati huo huo Gregory  amesema kuwa katika wilaya ya makete kuna nafasi 12 za wenyeviti wa vitongoji ziko wazi na nafasi 11 za wenyeviti wa  vijiji ziko wazi kama halmashauri inajipanga kufanya uchaguzi sehemu hizo na kuwapata  viongozi kwa mujibu wa sheria.

Gregory amesema uchaguzi wa marudio  utafanyika mpaka pale tume ya taifa ya uchaguzi itakapo toa taarifa za  kufanyika uchaguzi huo wa udiwani.


Share this article :

0 comments:

Post a Comment

 
Support : Copyright © 2018. AFRICAN NEWS BLOG - All Rights Reserved
Imetengenezwa na Edwin Moshi
Inaendeshwa na AFRICAN NEWS BLOG