Home » » OmbaOmba Kutupwa Gerezani

OmbaOmba Kutupwa Gerezani

Unknown | Sunday, April 08, 2018 | 0 comments

Mamlaka katika mji mkuu wa Rwanda, Kigali imetangaza kuanza msako mkali na kuwaweka gerezani walemavu wote wanaojihusisha na vitendo vya kuomba omba barabarani, kwa madai kuwa ni chanzo cha uchafu wa jiji hilo.

 Msako huo unaweza kutekelezwa wakati wowote kuanzia sasa, umewaonya walemavu hao kuwa kama hawataacha kuomba omba watakabiliwa na kifungo.

Baadhi ya wananchi wamepinga uamuzi huo wakisema, unalenga kukandamiza walemavu na watu masikini ambapo mashirika ya kiraia nchini Rwanda yameshauri kwamba kabla ya utekelezaji wa msako huo yafanyike mazungumzo ya pande zote.

Ripoti mbalimbali zimekuwa zikiitaja Kigali kuwa miongoni mwa majiji masafi barani Afrika huku ripoti nyingine hususani zile za kutetea haki za binadamu, zikiishutumu serikali kwa kuwafunga watu wasiojiweza.

Advertisement
Usipitwe na Habari Yoyote. Install Mpekuzi App kwenye Simu Yako Upate Habari Zetu kwa Wepesi Zaidi

==>>... << BOFYA HAPA  Kui Install>>
==
Share this article :

0 comments:

Post a Comment

 
Support : Copyright © 2018. AFRICAN NEWS BLOG - All Rights Reserved
Imetengenezwa na Edwin Moshi
Inaendeshwa na AFRICAN NEWS BLOG