Home » » Dr. Cheni Afunguka Mazito Kuhusu Maisha Ya Lulu Gerezani

Dr. Cheni Afunguka Mazito Kuhusu Maisha Ya Lulu Gerezani

Unknown | Sunday, April 08, 2018 | 0 comments
Muigizaji mkongwe wa Bongo movie Dr. Cheni  amefunguka mazito juu ya maisha ya Elizabeth Michael ‘Lulu’ gerezani.

Ni miezi kadhaa tangu Lulu aende jela baada ya kuhukumiwa miaka miwili baada ya kupatikana na hatia ya kumuua bila kukusudia aliyekuwa mpenzi wake marehemu Steven Kanumba.

Wiki iliyopita tuliona jinsi Dr. Cheni alivyomuwakilisha Lulu kwa kutoa msaada kwenye kampenzi ya Namthamini ya EATV. Dr. Cheni ni mtu ambaye siku zote amekuwa na ukaribu sana na Lulu hadi Lulu humuita Baba yake.

Kwa mara nyingine Tena Dr. Cheni amefunguka kuhusu maisha ya Lulu gerezani ambapo kwenye mahojiano na Millard Ayo Tv amefunguka haya:

 "Kusema ukweli Lulu ni binti jasiri sana yaani sisi tuliokuwa nje tuna majonzi kuliko yeye mwenyewe 

"Yaani ukienda unamkuta ana furaha mtacheka naye mtafurahi, kikubwa anasema tu niombeeni basi na kitu kikubwa Lulu huko jela anatizama sana mabinti, anasema anawapenda sana mabinti wa Kitanzania”.

Lakini pia Dr. Cheni amesema kuwa Lulu  ana kawaida sana ya kutoa misaada ingawa hapendi kujitangaza Kwenye mitandao ya kijamii pia amedai Miezi michache kabla hajahukumiwa alienda kutoa msaada segerea.

Advertisement
Usipitwe na Habari Yoyote. Install Mpekuzi App kwenye Simu Yako Upate Habari Zetu kwa Wepesi Zaidi

==>>... << BOFYA HAPA  Kui Install>>
==
Share this article :

0 comments:

Post a Comment

 
Support : Copyright © 2018. AFRICAN NEWS BLOG - All Rights Reserved
Imetengenezwa na Edwin Moshi
Inaendeshwa na AFRICAN NEWS BLOG