Home » » WAANDISHI WA HABARI REDIO ZA JAMII TANZANIA WAENDELEA NA MAFUNZO MJINI DODOMA

WAANDISHI WA HABARI REDIO ZA JAMII TANZANIA WAENDELEA NA MAFUNZO MJINI DODOMA

Unknown | Wednesday, February 07, 2018 | 0 comments



Waandishi wa habari wa radio za Kijamii nchini Tanzania wametakiwa kuzingatia maadili ya taaluma zao ili kuandika habari zenye weledi katika kuzisaidia jamii zinazowazunguka.
Wito huo umetolewa leo mjini Dodoma na Mkufunzi wa musuala ya habari kutoka shirika la Umoja wa mataifa la elimu, sayansi na utamaduni(UNESCO) Bi. Rose Haji Mwalimu kwenye mafunzo ya siku nane yanayoendelea kwenye ukumbi  wa wakala wa majengo (TBA).
Bi. Rose amesema ili jamii inufaike na uwepo wa radio za Kijamii, waandishi wa habari wanatakiwa kuzingatia miiko na misingi inayowaongoza katika Kutekeleza majukumu yao  kwa manufaa ya umma na wao binafsi.
Kwa upande wao waandishi wa habari wa radio za kijamii wamelishukuru shirika la UNESCO na kuongeza kuwa mafunzo hayo yatawasidia katika kuboresha utendaji wao wa kazi katika vituo vyao.
Shirika la unesco linaeendelea kutoa mafunzo ya uandishi wa habari kwa radio za kijamii nchini  ili kuwajengea uwezo wa kuandaa habari na vipindi vyenye ubora.

tazama picha za washiriki:-

 










Share this article :

0 comments:

Post a Comment

 
Support : Copyright © 2018. AFRICAN NEWS BLOG - All Rights Reserved
Imetengenezwa na Edwin Moshi
Inaendeshwa na AFRICAN NEWS BLOG