Home » » Ujumbe wa Lowassa kwa watanzania wanapoanza mwaka 2018

Ujumbe wa Lowassa kwa watanzania wanapoanza mwaka 2018

Unknown | Monday, January 01, 2018 | 0 comments
Aliyekuwa Waziri Mkuu wa Tanzania, Edward Lowassa, ametuma salamu za mwaka mpya kwa Watanzania, akiwasihi kuwa, wakati wanaposherehekea mwaka mpya wasikubali kugawanywa.

Lowassa ambaye pia ni mjumbe wa Kamati Kuu ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo, (CHADEMA) amesema kuwa amani na mshikamano nndio nguzo muhimu kwa Watanzania.

“Tunapouanza mwaka huu mpya, niwaombe watanzania wenzangu tukatae kugawanywa kwa sababu yoyote ile.
Umoja na mshikamano ndio nguzo yetu.”

Kwa siku za hivi karibuni, Lowassa ambaye ni miongoni mwa wanasiasa wakongwe nchini, amekuwa kimya, bila kuzungumzia masuala mbalimbali yanayoibuka katika siasa za Tanzania.

Advertisement
==
Share this article :

0 comments:

Post a Comment

 
Support : Copyright © 2018. AFRICAN NEWS BLOG - All Rights Reserved
Imetengenezwa na Edwin Moshi
Inaendeshwa na AFRICAN NEWS BLOG