Home » » SHULE YA SEKONDARI ISAPULANO YAANZA KAZI RASMI

SHULE YA SEKONDARI ISAPULANO YAANZA KAZI RASMI

Unknown | Thursday, January 25, 2018 | 0 comments


Mkuu wa shule ya sekondari ISAPULANO Mwl. METHOD SANGA shule iliyoko wilayani Makete  mkoani Njombe ameeleza kuridhishwa na mapokezi ya wananchi wa kata ya Isapulano hususani wananchi wa kijiji cha Isapulano kwa ushirikiano walio toa tangu kuanza Rasmi kwa shule hiyo Januali 8 mwaka huu.

Mwl Sanga amesema shule ya sekondari ISAPULANO yenye namba za usajili  S1050 nishule ya mkondo mmoja inajumla ya wanafunzi 39 wakiwemo wavulana 22 na wasichana 17 imeanza rasmi Januari 8 2018 ikiwa na walimu watatu huku mazingira ya kujifunzia yakiwa rafiki kwa wanafunzi na walim hasa katika upande wa miundombinu.

Aidha mkuu huyo amewashukuru wadau wa elimu ikiwemo Halmashauri ya wilaya Mbunge wa jimbo la Makete Prof Norman Adamson Sigara king,Diwani wa kata ya Isapulano wa fanyabiashara wa ndani na nje ya isapulano pamoja na wananchi wa kijiji cha Isapulano  kwa usirikiano walio utoa hadi kufanikisha shule kupata usajili na kuanza rasmi .
Mwl CHIKU MDINDILE ni miongoni mwa walimu wanaofundisha shule ya sekondari Isapulano amesema wamejipanga kuhakikisha shule hiyo inapata sifa nzuri kwa kufanya vizuri kitaaluma kwakuwa ipo katika mazingira mazuri na wananchi wamehamasika katika kuijenga shule yao huku wakitoa ushirikiano mkubwa hasa katika mambo yakijamii.

Wakizungumzia baadhi ya changamoto wanazokumbananazo walimu wa shule ya sekondari Isapulano wamesema nyumba za walimu maabara pamoja na baadhi ya vitendea kazi hasa kwa upende wa vitabu na vifaa vya maabara kwasasa  nivichache ambapo ameomba wadau wa elimu kuendelea kujitolea kwaajiliya kutatua changamoto hizo muda mufupi kabla ya kuaanza silabasi.

Baadhi ya wanafunzi wametoa wito kwa jamii na serkali kwa ujumla kuendelea kujenga shule hiyo ili kutengeneza mazingira rafiki kwao pamoja na walimu huku wakieeleza kufurahishwa na uwepo wa shule hiyo kwakuwa imewapunguzia Gharama na muda wakufuata mahitaji  makwao ambapo hapo awali walishuhudia ndugu zao wakiwapeleka watoto wao shule za mbali na kushindwa kumudu huduma muhimu kwa wanafunzi.










Pamoja na jitihada za wananchi wa kijiji cha isapulano kujenga shule nzuri likini miundombinu ya barabara kwao imekuwa tatizo hivyo wananchi hao wameomba serkali pamoja na wadau wengine kufukia sehem korofi katika barabara ya makete kupitia vijiji vya luvulunge na Isapulano kwenda Mbeya ili kurahisisha mawasiliano ya barabara kwa wanafunzi na jamii nzima kwa ujumla.


 hii ni sahem mojawapo korofi katika barab ara ya Isapulano.
Share this article :

0 comments:

Post a Comment

 
Support : Copyright © 2018. AFRICAN NEWS BLOG - All Rights Reserved
Imetengenezwa na Edwin Moshi
Inaendeshwa na AFRICAN NEWS BLOG