Home » » Maria na Consolata Mwakikuti wamelazwa Hospitali ya Rufaa ya Iringa kwa matibabu ya moyo.

Maria na Consolata Mwakikuti wamelazwa Hospitali ya Rufaa ya Iringa kwa matibabu ya moyo.

Unknown | Monday, January 01, 2018 | 0 comments
Pacha walioungana Maria na Consolata Mwakikuti wanaosoma mwaka wa kwanza Chuo Kikuu cha Kikatoliki cha Ruaha (Rucu), wamelazwa katika Hospitali ya Rufaa ya Iringa kwa matibabu ya moyo.
Kaimu Mganga Mfawidhi wa hospitali hiyo, Dk Alfred Mwakalebela amesema hali zao zinaendelea vizuri ikilinganishwa na juzi walipofikishwa hapo.
Dk Mwakalebela amesema leo Jumamosi Desemba 30,2017 kuwa pacha hao wapo chini ya uangalizi wa daktari bingwa wa magonjwa ya moyo.
“Wanaendelea vizuri tunamshukuru Mungu, tayari daktari bingwa wa moyo anaendelea kuwapa matibabu,” amesema Dk Mwakalebela.
Maria na Consolata walijiunga na Rucu mwaka huu baada ya kuhitimu kidato cha sita katika Shule ya Sekondari ya Udzungwa wilayani Kilolo mkoani Iringa.
Wanalelewa chini ya uangalizi wa Serikali ya Mkoa wa Iringa na Rucu kwa sasa. Awali, walikuwa chini ya masista wa Shirika la Maria Consolata lililowalea na kuwasomesha tangu wakiwa wadogo.
Na Tumaini Msowoya, Mwananchi
Share this article :

0 comments:

Post a Comment

 
Support : Copyright © 2018. AFRICAN NEWS BLOG - All Rights Reserved
Imetengenezwa na Edwin Moshi
Inaendeshwa na AFRICAN NEWS BLOG