Home » » Y-JAY AZUNGUMZIA MUZIKI WA KIZAZI KIPYA KATIKA SURA YA MPYA

Y-JAY AZUNGUMZIA MUZIKI WA KIZAZI KIPYA KATIKA SURA YA MPYA

Unknown | Wednesday, January 03, 2018 | 0 comments

Msanii wa muziki wa kizazi kipya Ahazi Ndelwa Lusemba  (Y-Jay) kutoka Makete Mkoani Njombe ameelezea mazingira kuwa kikwazo cha wasanii wa mikoani kuweza kuendana na kasi ya soko la muziki na ushindani mkubwa uliopo kwa sasa.
Y-Jay ameyasema hayo alipokuwa akizungumza na AFRICAN NEWS BLOG wakati alipotakiwa kueleza sababu za kutoachia kazi kwa kasi kulingana na ushindani uliopo,

Aidha kutokana na mazingira kutokuwa na fulsa kimuziki na kutumia gharama kubwa kutafuta soko la muziki na kufanya promotion kwake na wasanii wa mikoani amewaasa wasanii kufanya maandalizi kabla ya kuingia kwenye soko la ushindani.

Hata hivyo kwa mwaka 2018 amesema kwa siku zijazo anatarajia kuachia kazi mpya itakayo kwenda kwa jina la NITULIE,

Y - JAY Ni miongoni mwa wasanii kutoka Mkoani Njombe ambaye kwasasa anafanya vizuri na nyimbo tatu , pigo la moyo,fadhira na Show Love amewataka wadau  wa muziki kutambua umuhim wa sanaa na kusaport kazi za wasanii wa Mikoani. 


 <ihttps://youtu.be/tyfIvfZ68Ps
Share this article :

0 comments:

Post a Comment

 
Support : Copyright © 2018. AFRICAN NEWS BLOG - All Rights Reserved
Imetengenezwa na Edwin Moshi
Inaendeshwa na AFRICAN NEWS BLOG