Home » » wanahabari wa dhamilia kuleta mabadiliko kwa jamii ya Tanzania

wanahabari wa dhamilia kuleta mabadiliko kwa jamii ya Tanzania

Unknown | Friday, December 01, 2017 | 0 comments


Shirikala la umoja wa mataifa linalo shughurika  na Elimu ,sayansi na Utamaduni (UNESCO) imeendelea kuwajengea uwezo waandishi wa habari kutoka katika Redio za jamii nchini juu yaTathimini na ufuatiliaji  (Monitoring  and Evaluation) lengo likiwa ni kuibua na kutafutia ufumbuzi changamoto zinazo ikabili jamii ya kitanzania kupitia vipindi na habari zenye kuleta matokeo chanya .

Mwezeshaji kutoka UNESCO Bw,MARCO GIDEON ametoa wito kwa washiriki kufanya kazi kwa kufuata kanuni , miongozo na maadili katia taaluma ya habari ili kuendana na malengo ya milenia hadi ifikapo mwaka 2030 ambapo amesema shirika limelenga kujengea uwezo Redio za jamii ili kuibua na kutafutia ufumbuzi wa changamoto zinazo ikabili jamii.

Baadhi ya washiriki wa mafunzo  ya tathimini na ufuatiliaji (M&E )kutoka redio mbalimbali wameishukuru UNESCO kwa mafunzo wanayoyatoa kwa redio za Jamii huku wakiomba shirika kuendelea na miradi ya kuwajengea uwezo waandishi wa habari ili kuleta mabadiliko chanya kwa jamii.

Revocutus Msafiri ni miongoni mwa washiriki wa semina hiyo amesema mafunzo yanayotolewa na UNESCO yameleta matokeo kwa redio za jamii ikiwemo waandishi wa habari kupata uzoefu katika uandaaji na ufanyaji wa vipindi na habari huku akitoa rai kwa vyombo vingine pamoja na wadau wa  habari kushirikiana katika kubuni miradi itakayo ibua changamoto na kuzitafutia majibu yatakayopelekea kuibadilisha jamii pamoja na kuleta maendeleo.

Aidha mafunzo hayo yametolewa na shirika la UNESCO yakihusisha redio za jamii kutoka Tanzania Bara na Visiwani huku washiriki wote wakionyesha kuridhika na mafunzo hayo.
Share this article :

0 comments:

Post a Comment

 
Support : Copyright © 2018. AFRICAN NEWS BLOG - All Rights Reserved
Imetengenezwa na Edwin Moshi
Inaendeshwa na AFRICAN NEWS BLOG