Home » » Tundu Lissu: Kushambuliwa kwangu kulichochewa na siasa Tanzania

Tundu Lissu: Kushambuliwa kwangu kulichochewa na siasa Tanzania

Unknown | Friday, December 01, 2017 | 0 comments

Image result for picha za lisu akiwa nairobi hospitali

Mwanasheria kuu wa chama upinzani Chadema nchini Tanzania Tundu Lissu, ambaye amekuwa akipokea matibabu Nairobi tangu alipopigwa risasi na watu wasiojulikana jijini Dodoma mwezi Septemba, amesema anaamini kushambuliwa kwake kulihusiana na siasa nchini humo.
Akizungumza na BBC, mbunge huyo wa Singida Mashariki amelilaumu Bunge la nchi hiyo akisema halijachukua hatua zozote kumsaidia tangu kulazwa kwake hospitalini.
Makamu wa Rais wa Tanzania Bi Samia Suluhu alimtembelea hospitalini mapema wiki hii.
Bw Lissu amesema anaendelea kupata nafuu vyema.
Juhudi za BBC za kuwasiliana na msemaji wa Bunge la Tanzania kuhusu tuhuma za Bw Lissu hazijafua dafu.
Amezungumza na mwandishi wa BBC John Nene.
Share this article :

0 comments:

Post a Comment

 
Support : Copyright © 2018. AFRICAN NEWS BLOG - All Rights Reserved
Imetengenezwa na Edwin Moshi
Inaendeshwa na AFRICAN NEWS BLOG