Home » » TAKUKULU YATOA MAFUNZO KWA WAKUU WA IDARA HALMASHAURI YA WILAYA YA MAKETE

TAKUKULU YATOA MAFUNZO KWA WAKUU WA IDARA HALMASHAURI YA WILAYA YA MAKETE

Unknown | Thursday, December 07, 2017 | 0 comments



Ikiwa tar 10 ni siku ya kilele cha  maadili  duniani elimu imetolewa  juu ya kutoa na kupokea Rushwa  na Taasisi ya kuzuia na kupambana na Rushwa Takukuru  kwa wakuu wa Idara wilayani makete mkoani njombe na   .
Elimu hiyo imetolewa  mapema hii leo katika ukumbi wa halmashauri bwana Emmily Okelo wa ofisi ya kupambana na rushwa [Takukuru] wilayani makete kwa niaba ya mkuu wa takukuru wilaya amesema katika kilele cha kuazimisha siku ya maadili ambayo inaazimishwa  kaunzia tar 6 disember hadi tar 10 ya mwezi desemba ambapo ndo kilele cha maadhimisho hayo
Bwana OKELO amewataka wakuu wa idara mbalimbali katika halmashauri ya wilaya ya makete kuwa na wajibu wa kulinda Rasilimali fedha na vifaa huku  kauli mbiu yake kwa mwaka huu  ikiwa inasema  wajibika pinga vitaRushwa,zingatia maadili,haki za binadamu kuelekea uchumi wakati.
Pia amesema  wananchi na wafanyakazi wanatakiwa kufuata maadili na utii wa sheria ya kuzuia na kupambana na rushwa  TAKUKURU  sheria namba 11 ya mwaka 2017 na wananchi wanatakiwa kuisoma ili kuielewa vizuri.
Ofisi ya takukuru  Imesema  wananchi na wafanyakazi  wanahaki na wajibu  wa kutembelea ofisi ya kupambana  na rushwa Takukuru kujifunza baadhi ya vitu, kuomba ushauri,na mapendekezo na watayapokea kwa kuyafanyia kazi.
Naye mkurugezi wa  halmashauri ya wilaya ya makete Ndugu Francis E Namaumbo amewashukuru ofisi ya kupambana na rushwa takukuru kwa kutoa elimu na amewashauri wafanyakazi na wananchi kutoa ushirikiano kwa ofisi hiyo  kwa kuwapa mialiko mbalim bali ili kuweka ukaribu nao.


Share this article :

0 comments:

Post a Comment

 
Support : Copyright © 2018. AFRICAN NEWS BLOG - All Rights Reserved
Imetengenezwa na Edwin Moshi
Inaendeshwa na AFRICAN NEWS BLOG