Home » » AHUKUMIWA KWA KUMFANYIA UKATILI MTOTO WA MIAKA (11) BULONGWA MAKETE NJOMBE

AHUKUMIWA KWA KUMFANYIA UKATILI MTOTO WA MIAKA (11) BULONGWA MAKETE NJOMBE

Unknown | Thursday, December 07, 2017 | 0 comments




Mahakama ya mwanzo Makete imemhukum Bi, HURUMA KYANDO (26) mkinga mkulima,mkristo mkazi wa kijiiji cha Bulongwa wilaya ya Makete mkoani Njombe kulipa faini ya shilingi milioni moja (1000,000/=)au kutumikia kifungo gerezani miezi sita na fidia ya shilingi laki mbili kwa kosa  la kumfanyia ukatili mtoto wa miaka 11 aneyesoma darasa la tano shule ya msingi Bulongwa.
Mshitakiwa alitenda kosa hilo la kumfanyia ukatili mtoto kinyume na kifungu cha 21 na 14 cha sheria ya mtoto namba 21 ya mwaka 2009.
Kosa hilo lilitendeka mnamo tarehe 25/11/2017 huko katika kijiji cha Bulongwa ambapo mshitakiwa alimtumbukiza mtoto huyo kwenye shimo la choo kwa kumfunga kamba ya manira tumboni kwa lengo la kumtoa mbuzi aliyekuwa ametumbukia katika shimo hilo hivyo kumsababishia maumivu makali na kuhatarisha uhai wake.
Baada ya kusomewa shitaka hilo mtuhumiwa alikili kutenda kosa hilo hivyo mahakama kumtia hatihani na kutoa hukum hiyo.
Share this article :

0 comments:

Post a Comment

 
Support : Copyright © 2018. AFRICAN NEWS BLOG - All Rights Reserved
Imetengenezwa na Edwin Moshi
Inaendeshwa na AFRICAN NEWS BLOG