Home » » Chimbuko la Illuminati na dhana kuhusu nguvu zao

Chimbuko la Illuminati na dhana kuhusu nguvu zao

Unknown | Wednesday, December 06, 2017 | 0 comments

Ni simulizi ya ulaji njama ambayo bila shaka imevuma zaidi kushinda njama nyingine zote. Ni wachache sana ambao hawajawahi kusikia kuwahusu Illuminati.
Huaminika kuwa kundi maalum la watu ambao hudhibiti masuala na uongozi wa dunia, na inasadikika kuwa hufanya shughuli zao kisiri kudhibiti kila kitu na kuunda Utawala Mpya wa Dunia.
Kwa wengine, wamehusishwa na utajiri wa ghafla ambao si wa kawaida.
Ukitajirika haraka, kunao bila shaka watakaodai kwamba umejiunga na Illuminati.
Je, kuna ukweli wowote kuhusu wasiwasi huu? Kuna kundi la watu wanaofanya vikao vya siri kupanga njama za kuitawala dunia na pia kjifaidi wenyewe kwa pesa na utajiri?
Simulizi hizi na umaarufu wa illuminati zina ukweli wowote?
Wasiwasi huu kuhusu kundi linalopanga njama ya kuweka utawala mpya duniani ulianza miaka ya 1960, sana kutokana na ubunifu wa watu fulani.
Kuenea kwa habari hizo kunatoa viashiria fulani kuhusu jinsi binadamu walivyo tayari kuamini mambo wanayoyasikia au kuyasoma, kwa urahisi sana. Aidha, kunaweza kutoa funzo kuu kuhusu taarifa na habari za uongo ambazo zinaenezwa mtandaoni siku hizi.
Kwa kuchunguza kuhusu historia ya illuminati, kwa kuanzia huwa ni nchini Ujerumani, Enzi za Kuelimika au Kustaarabika barani Ulaya (1685-1815) ambapo kulikuwa na kundi lililofahamika kama Kundi la Illuminati.
Lilikuwa ni kundi la usiri sana ambalo lilianzishwa mwaka 1776 katika eneo la Bavaria.
Wanachama wake walikuwa watu walioelimika na wasomi na kusudi lao lilikuwa kuungana na kupinga pamoja na kukabiliana na ushawishi wa makundi ya kidini na wasomi wengine katika maisha ya kawaida ya kila siku.
Kundi hilo liliwajumuisha watu kadha
Ilikuwa ni hadi miaka ya 1960 ambapo walianza kutajwa tena.
maarufu waliokuwa wasomi au wapenda maendeleo wakati huo. Kulikuwa pia na wanachama wa Freemason (wamasoni).
Walijipata wakipingwa vikali na makundi ya wahafidhina na Wakristo na mwishowe kupigwa marufuku. Ushawishi wao ulififia na hawakusikika tena kwa muda mrefu.

Share this article :

0 comments:

Post a Comment

 
Support : Copyright © 2018. AFRICAN NEWS BLOG - All Rights Reserved
Imetengenezwa na Edwin Moshi
Inaendeshwa na AFRICAN NEWS BLOG